KIKUNDI KINGINE CHA NGOMA ZA ASILI KUTOKA MKOA WA MARA CHAENDA KUSHINDANA NJE YA MKOA WAO
MATUMIZI YA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO YAJADILIWA HADHARANI
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL – WANAVIJIJI WAKUBALIANA KUONGEZA KASI YA UJENZI
UJENZI WA DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL WAENDELEA VIZURI

PROF MUHONGO ATUNUKIWA HATI YA HESHIMA

Msaidizi wa Mbunge, Ndugu Fedson Masawa akipokea HATI ya HESHIMA kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo. Mbunge wa Jimbo hakuwepo kwani alikuwa kwenye maziko ya Marehemu Mhe Balozi Paul James Ndobho.
Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya Musoma Vijijini leo September 14, 2019 imemtunuku HATI ya HESHIMA Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo.
Ndugu Julius Kambarage Masubo, Mjumbe wa Baraza la Wazazi Taifa kutoka Mkoa wa Mara ndiye aliyekuwa MGENI RASMI wa Baraza la Wazazi Wilaya ya Musoma Vijijini lililokutana leo Kijijini Chumwi
Akikabidhi HATI hiyo, MGENI RASMI amesema, “HATI hii ni Ishara ya kipekee ya kutambua Mchango na Utendaji kazi mzuri na uliotukuka wa Mbunge wa Jimbo katika kuitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2015 – 2020 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.
Mgeni Rasmi huyo aliendelea kusema kwamba, HATI hiyo ni kielelezo cha kutambua MCHANGO MKUBWA wa Mbunge huyo kwenye Chama (CCM) na Jumuiya zake zote.
Ndugu Kambarage Masubo ametoa pongezi nyingi kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Muhongo kwa Uongozi Shirikishi unaowaunganisha Wananchi wa Musoma Vijijini katika kuharakisa Maendeleo Jimboni mwao.
Jimbo hili halina malumbano ya kisiasa wala halina mivutano ya kikabila – Mbunge wa Jimbo wanawaunganisha Wananchi wote kwenye MIRADI ya Maendeleo bila ubaguzi wa aina yo yote ile.
Wengine waliotunukiwa HATI ya HESHIMA na Jumuiya ya Wazazi ni pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma, Mhe Charles Magoma Nyambita pamoja na Diwani wa Kata ya Bukima Mhe January Simula.
Ndugu Kambarage Masubo ameikumbusha Jumuiya ya Wazazi wawe kitu kimoja kuhakikisha Ilani ya Chama cha Mapinduzi inatekelezwa kwa kasi kubwa chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt John Joseph Pombe Magufuli.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Musoma Vijijini, Ndugu Phares Maghubu amesisitiza kuwa Jumuiya ya Wazazi inaendelea kuimarisha mipango yao ya utunzaji wa Mazingira, kuhamasisha uboreshaji wa elimu na kuimarisha nidhamu na maadili kwa Vijana ili kuwa na kizazi chenye maadili mazuri na chenye kujituma katika shughuli za ki-uchumi na maendeleo.
CHAMA CHA MAPINDUZI KATA YA RUSOLI YAMTUNUKU MHE. MBUNGE WA JIMBO HATI YA HESHIMA.
WANANCHI WA KIJIJI CHA KABURABURA NAO WAAMUA KUJENGA ZAHANATI YAO
VIKUNDI VYA WATU WENYE ULEMAVU VYANUFAIKA NA MIKOPO KUTOKA HALMASHAURI NA BMZ
VIJANA WANUFAIKA NA KILIMO CHA BUSTANI KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO
UJENZI, UKAMILISHAJI NA UBORESHAJI WA MAABARA ZA MASOMO YA SAYANSI KWENYE SEKONDARI ZA KATA
WAZAZI WA KATA YA TEGERUKA WAAGA VIJANA WAO KWA ZAWADI YA KIPEKEE
MIRADI MIKUBWA YA MAJI INAYOTEKELEZWA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJI
VIJIJI VIWILI VYA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI VYAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAO
SHULE YA MSINGI MURANGI – SOMO LA STADI ZA KAZI LATUMIKA KUIMARISHA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
BOMBA LA MAJI SAFI NA SALAMA – MRADI WA MUGANGO-KIABAKARI-BUTIAMA
MIRADI YA SEKTA YA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

baadhi ya MAJENGO ya Hospitali ya Wilaya inayojengwa Jimboni mwetu (Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti). DC, DED, MADIWANI na Wafanyakazi wa Halmashauri yetu WAPEWE PONGEZI nyingi sana kwa usimamiaji mzuri wa ujenzi wa Hospitali hii
Jimbo lina Kata 21, Vijiji 68, Vitongoji 374
ZAHANATI
* 24 za Serikali zinazotoa huduma
* 4 za Binafsi zinatoa huduma
* 13 MPYA zimeanza kujengwa na Wanavijiji wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
VITUO VYA AFYA
* 2 vya Serikali vinavyotoa huduma za Afya (Murangi & Mugango)
* 1 KIPYA kimeanza kujengwa na Wanavijiji (Kata ya Nyambono) wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
HOSPITALI YA WILAYA
* Inajengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti
* Serikali imetoa Tsh 1.5 bilioni kuanza ujenzi wake
* Kila Kijiji kimekubali kuchangia Tsh Milioni 2.
* Mbunge wa Jimbo amekubali kuchangia
ZAHANATI ZINAZOJENGWA NA WANAVIJIJI
(1) Kitongoji cha Burungu, Kijijini Bukumi, Kata ya Bukumi
(2) Kijijini Butata, Kata ya Bukima
(3) Kijijini Chimati, Kata ya Makojo
(4) Kijijini Chirorwe, Kata ya Suguti
(5) Kijijini Kakisheri, Kata ya Nyakatende
(6) Kijijini Kurwaki, Kata ya Mugango
(7) Kijijini Maneke, Kata ya Busambara
(8) Kijijini Mkirira, Kata ya Nyegina
(9) Kijijini Kurukerege, Kata ya Nyegina
(10) Kijijini Nyegina, Kata ya Nyegina
(11) Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro
(12) Kijijini Bwai Kwitururu, Kata ya Kiriba
(13) Kijijini Nyasaungu, Kata ya Ifulifu
WANAFUNZI WA NYAMBONO SECONDARY SCHOOL WAFURAHIA MADAWATI YALIYOTOLEWA NA BENKI YA NMB
UONGEZAJI WA HIGH SCHOOLS NA UBORESHAJI WA ELIMU YA SAYANSI KWENYE SEKONDARI ZETU
WAFUGAJI WAAMUA KUTUMIA MIFUGO YAO KUCHANGIA UJENZI WA SEKONDARI MPYA, ZAHANATI NA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE YA MSINGI
SEKONDARI MOJA YA KATA HAITOSHI – WANANCHI WAAMUA KUJENGA SEKONDARI YA PILI
UKARABATI WA MABWENI YA SEKONDARI YA BWASI
MBEGU YA MIHOGO YA AINA YA MKOMBOZI YANUFAISHA WAKULIMA JIMBONI
HALMASHAURI YASHIRIKIANA NA MRADI WA BMZ (Ujerumani) KUTOA HUDUMA KWA VITUO VYA ELIMU YA WATOTO WENYE ULEMAVU
UJENZI WA SHULE SHIKIZI MWALONI KIJIJINI BURAGA UNAENDELEA VIZURI
WANAKIJIJI NA SERIKALI KUPITIA MRADI WA EQUIP WAKAMILISHA UJENZI WA SHULE SHIKIZI MWIRINGO
MRADI WA USAMBAZAJI WA MAJI WATEKELEZWA KWENYE VIJIJI VITANO (5)
KIKUNDI CHA NGUVUKAZI CHATOA MSAADA WA CHAKULA SHULENI
KILIMO CHA UMWAGILIAJI CHANUFAISHA KIUCHUMI KIKUNDI CHA MKULIMA JEMBE CHA KATA YA BUKIMA
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA AFYA WAPAMBA MOTO JIMBONI
SERIKALI YASAIDIA SHULE YA MSINGI KIRIBA KWENYE UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA NA UPATIKANAJI WA MADAWATI
KIJIJI CHA NYASAUNGU WATUMIA WIKI 1 KUKAMILISHA MSINGI WA SEKONDARI WANAYOIJENGA
SERIKALI YAPIGA JEKI WANAKIJIJI KWENYE KATA YA BUGWEMA KUJENGA SHULE SHIKIZI
ELIMU YA KILIMO SHULENI – SHULE YA SEKONDARI NYANJA YAANZA KUTOA ELIMU YA KILIMO CHA ALIZETI KWA WANAFUNZI WAKE
MKURUGENZI KAYOMBO ATOA MIKOPO YENYE THAMANI YA SHILLINGI MILLIONI 11 KWA VIKUNDI VYA KWIKUBA CARPENTRY NA AMANI NA UPENDO, HALMASHAURI YAFIKIA ASILIMIA 92.6 YA LENGO LA UTOAJI MIKOPO KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019*.
SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI – KIJIJI CHA NYEGINA CHAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAKE
SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI: KATA YA KIRIBA IMEANZA UJENZI WA MIUNDOMBINU KWENYE SHULE ZAKE KWA KASI MPYA
EID EL FITR NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – SHEREHE NA MAENDELEO VIJIJINI
UKAGUZI WA UJENZI WA HOSPITAL YA WILAYA
SHIRIKA LA BMZ LAENDELEA KUWAWEZESHA WATU WENYE ULEMAVU NA WANAFUNZI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
KITONGOJI CHA RWANGA CHAENDELEA KWA KASI KUBWA KUJENGA SHULE YAKE YA MSINGI
WANAKAZI WA KIJIJI CHA KAKISHERI WACHOSHWA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA HUDUMA ZA AFYA
UJENZI WA SHULE SHIKIZI YA KIJIJI CHA BUANGA WAFIKIA HATUA NZURI
DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL – KUANZA KUCHUKUA WANAFUNZI WA FORM I JANUARY 2020
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL
UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MKIRIRA WAENDELEA VIZURI
WAZALIWA WA KATA YA NYAMBONO WATEKELEZA AHADI ZAO KWA VITENDO: JENGO LA OPD LA KITUO CHA AFYA NYAMBONO LAKARIBIA KUEZEKWA
KILIMO CHA UMWAGILIAJI CHAANZA KUWEKEWA MKAZO JIMBONI MWETU
UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO: SERIKALI NA WANANCHI WAENDELEA KUSHIRIKIANA KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA KIJIJINI SUGUTI WAENDELEA VIZURI
WANANCHI WA KIJIJI CHA ETARO WAMEDHAMIRIA KUKAMILISHA UJENZI VYUMBA 5 VYA MADARASA IFIKAPO MWISHONI MWA MEI 2019
UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA MRADI WA SERIKALI WA EP4R WATEKELEZWA KIJIJINI CHIRORWE
WANAFUNZI 133 WA FORM I WA SHULE YA SEKONDARI BUKIMA WALIOSUBIRI UPATIKANAJI WA VYUMBA VYA MADARASA WAANZA MASOMO
MAKTABA YAZINDULIWA KISIWANI RUKUBA – ZAWADI YA PASAKA KWA WAKAZI WA KISIWA HICHO
WANANCHI WA KIJIJI CHA KABEGI WAAMUA KUJENGA SHULE SHIKIZI KWENYE KITONGOJI CHA BINYAGO
WANANCHI WA KISIWA CHA RUKUBA WAANZA MAANDALIZI YA UJENZI WA WODI YA MAMA NA WATOTO
WANAVIJIJI WALIKUBALI ZAO JIPYA LA BIASHARA LA ALIZETI JIMBONI MWAO
PAROKIA YA BUKIMA YAJENGA MAABARA YA KISASA YA VIPIMO VYA AFYA
WANANCHI WA KATA YA MUGANGO WAWA MFANO WA KUIGWA KWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO
SERIKALI YATOA SHILINGI MILIONI 146 KWENYE SHULE YA SEKONDARI KIRIBA
UJENZI NA UKAMILISHAJI WA MAABARA KWENYE SEKONDARI ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
JIWE LA MSINGI LA “DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL” KUWEKWA TAREHE 18.04.2019
WANANCHI KIJIJI CHA CHIMATI WAAMUA KUJENGA ZAHANATI YA KIJIJI CHAO
UJENZI WA SHULE SHIKIZI BUSAMBARA UMEPATA MSUKUMO MPYA BAADA YA KUSUASUA KWA MIEZI KADHAA
S/M RUKUBA YAKARIBIA KUKAMILISHA UJENZI WA MAKTABA YAO – MFANO WA KUIGWA NA SHULE NYINGINE
UFAULU MDOGO NA UMBALI MKUBWA WA SHULE ZA JIRANI VIMEWAFANYA WAKAZI WA KITONGOJI CHA MWALONI KUAMUA KUJENGA SHULE YAO
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – UJENZI WA ZAHANATI WAZIDI KUSHIKA KASI JIMBONI
MIRADI YA TANROADS NA TARURA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI YAKAGULIWA
MBUNGE ACHANGIA SARUJI KATIKA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA S/M RWANGA.
WANANCHI WA KIJIJI CHA WANYERE WAENDELEA NA UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA
WANANCHI WA KIJIJI CHA BUSUNGU WAAMUA KUTOKOMEZA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SHULE YAO YA MSINGI
KIJIJI CHA KAKISHERI CHAAMUA KUJENGA ZAHANATI YA KIJIJI CHAO
WANANCHI KIJIJI CHA NYABAENGERE WAMEAMUA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU KWENYE SHULE YAO YA MSINGI – KILA KITONGOJI KUJENGA DARASA MOJA
KATA YA BUKIMA WAAMUA KUTATUA TATIZO LA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA KWANZA
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWETU NI WA LAZIMA KUFANYIKA SASA NA KWA KASI KUBWA
WANAFUNZI 232 NDANI YA CHUMBA KIMOJA CHA DARASA – WANANACHI WAAMUA KUTATUA MATATIZO YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA MASHULEN
WANAFUNZI WA DARASA LA 7 JIMBONI WANAFAULU LAKINI WANACHAGULIWA WACHACHE KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI KUTOKANA NA UPUNGUFU MKUBWA WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI ZA KATA
WANANCHI WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI WAMEAMUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU JIMBONI MWAO
MBUNGE WA MUSOMA VIJIJINI AENDELEA KUSHIRIKIANA NA WANAVIJIJI JIMBONI KUJENGA NA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU
KIJIJI CHA BUIRA CHAONYESHA NJIA, CHAJENGA MAKTABA KWENYE SHULE YAKE YA MSINGI
WANAVIJIJI WA KATA YA KIRIBA – WASEMA – “HAKUNA MTOTO ALIYECHAGULIWA KWENDA FORM I ATAKAYEBAKI NYUMBANI KWA SABABU YA UKOSEFU WA VYUMBA VYA MADARASA KWENYE SEKONDARI YAO YA KATA.”
SHEREHE ZA KRISMASI ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI ZIMEFANYIKA KWENYE KANISA LA KATOLIKI KIJIJINI BUKUMI
KATA ZASHINDANA KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
PROF MUHONGO AOMBA JINA LAKE LIACHWE NA BADALA YAKE LICHUKULIWE JINA LA MAREHEMU JAJI DAN MAPIGANO
WANAFUNZI WAWILI TU WA KUTOKA KITONGOJI CHA BURAGA MWALONI NDIO WAMECHAGULIWA KUENDELEA NA MASOMO YA SEKONDARI – WAZAZI WACHARUKA NA KUAMUA KUJENGA SHULE YAO YA MSINGI
UBORESHAJI WA KILIMO CHA ZAO LA MIHOGO NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
MIUNDOMBINU YA ELIMU – UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
WANANCHI WA KIJIJI CHA CHIMATI WAMEAMUA KUPUNGUZA UHABA WA VYUMBA VYA MADARASA
SHULE SHIKIZI EGENGE YAKAMILIKA
BMZ WAKAMILISHA ZOEZI LA UGAWAJI WA VIFAA VYA ELIMU KWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU
UJENZI WA VYUMBA VINNE VYA MADARASA YA SHULE SHIKIZI YA MWIKOKO WAFIKIA HATUA NZURI
PROF MUHONGO ACHANGIA SARUJI SIKU YA MAHAFARI YA SHULE YA SEKONDARI SUGUTI

Prof Sospeter Muhongo amechangia Saruji Mifuko 50 kwenye Harambee ya kuchangia ukamilishaji wa ujenzi wa Jengo la Utawala wa Shule ya Sekondari Suguti.
Na Hamisa Gamba, Msaidizi wa Mbunge
WANANCHI WA KIJIJI CHA BUANGA KUKAMILISHA UJENZI WA SHULE JANUARI 2019
PROF MUHONGO ASHIRIKI HARAMBEE UJENZI WA BWENI LA WASICHANA LA SEKONDARI YA BWASI
VIKUNDI VYA BUSTANI KUTOA FURSA ZAIDI ZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
KILIMO CHA KISASA CHA WANANCHI WENYEWE NDANI YA BONDE LA BUGWEMA
WAZIRI WA NISHATI AKAGUA UTEKELEZAJI WA MRADI WA REA III JIMBONI

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akikagua Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini wa REA III ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini
Na Fedson Masawa, Msaidizi wa Mbunge
18 – 09 – 2018
WAZIRI wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amefanya ziara ya Ukaguzi wa Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini wa REA III ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini ambapo pia ametumia fursa hiyo kuzungumza na wananchi wa Jimbo hilo kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo Umeme Vijijini.
Akizungumza katika Mkutano wa hadhara leo Agosti 18, 2019 Kijijini Nyakatende, Dkt. Kalemani amewahakikishia wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini kwamba TAASISI, maeneo mbalimbali ya UWEKEZAJI na VITONGOJI vyote 374 vya Jimbo VITAPATA UMEME.
Awali akieleza kuhusu kero ya Umeme Musoma Vijijini, Waziri Kalemani amesisitiza kuwa Prof Muhongo aliomba Umeme kwenye Vijiji vyake vyote 68 na amepewa Vijiji vyote katika Mradi wa REA III
Akisisitiza juu ya jambo hilo, Dkt. Kalemani amesema kuwa kazi ya Mkandarasa ni kuhakikisha anapeleka umeme Vijiji vyote 68 vyenye VITONGOJI 374 katika awamu hii ya REA III
“Hakuna kijiji, hakuna kitongoji na hakuna mwananchi atakayerukwa katika Mradi huu” Amesisitiza Mhe Dkt. Kalemani
Aidha Waziri Dkt Kalemani ametoa maelekezo ya Uboreshaji wa Utekelezaji wa Mradi wa REA III mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Madiwani na WANANCHI wa Musoma Vijijini.
Dkt. Kalemani amewaagiza watendaji wake kufanya kazi bila kuondoka saiti hadi watakapokamilisha kazi hiyo.
“Mkandarasi nataka usihamishe genge, peleka genge kila kijiji. Badala ya kuhamishahamisha,” alisema Waziri wa Nishati Mhe Dkt Kalemani.
Vilevile, Dkt. Kalemani ameshiriki Tukio la Kuwasha Umeme Kijijini Nyakatende kuashiria Uzinduzi rasmi wa Mradi wa REA III Musoma Vijijini.
Katika Ziara yake hiyo, Dkt Kalemani aliongozana viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati na Taasisi zake ambao ni pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TANESCO, Kaimu Mtendaji Mkuu wa REA, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara, Engineer wa TANESCO Kanda ya Ziwa (Mwanza), Engineer wa Miradi ya REA Kutoka Makao Makuu, na Mkandarasi wa Mradi wa REA III Mkoa wa Mara.
Dkt. Kalemani amehitimisha ziara yake Jimboni kwa kutoa pongezi nyingi kwa Mbunge wa Jimbo, Prof Muhongo kwa Jitihada kubwa za Maendeleo anazozifanya. akishirikiana na Mkuu wa Wilaya, Dr. Vicent Naano na Viongozi wengine. Mhe Waziri amewataka Madiwani na Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha Jimbo la Musoma Vijijini linapiga hatua kubwa za kimaendeleo.