RATIBA YA KUMBUKIZI YA BABA WA TAIFA
SERIKALI YAENDELEA NA MATAYARISHO YA MRADI MKUBWA WA MAJI NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
KARIBU TUKAMILISHE MAJENGO YA DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL
KARIBUNI TUKAMILISHE UJENZI WA BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL
SEKONDARI ZAJITAYARISHA KWA ONGEZEKO LA WANAFUNZI MWAKANI (JAN 2020): VYUMBA VIPYA VYA MADARASA VINAHITAJIKA
WANAVIJIJI NA MBUNGE WAO WA JIMBO WAAMUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUHARAKISHA UJENZI WA HOSPITAL YA WILAYA YAO
MWITONGO, BUTIAMA: KABURI (MAUSOLEUM) LA BABA WA TAIFA LINAPAKWA RANGI NA KUSAFISHWA
JAMII IMPACT LIMITED YAKARIBISHA USHIRIKIANO NA VIKUNDI VYA UZALISHAJI
PROF MUHONGO AKAMILISHA AHADI YAKE YA SARUJI MIFUKO 100
KIKUNDI KINGINE CHA NGOMA ZA ASILI KUTOKA MKOA WA MARA CHAENDA KUSHINDANA NJE YA MKOA WAO
MATUMIZI YA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO YAJADILIWA HADHARANI
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL – WANAVIJIJI WAKUBALIANA KUONGEZA KASI YA UJENZI
UJENZI WA DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL WAENDELEA VIZURI

PROF MUHONGO ATUNUKIWA HATI YA HESHIMA

Msaidizi wa Mbunge, Ndugu Fedson Masawa akipokea HATI ya HESHIMA kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo. Mbunge wa Jimbo hakuwepo kwani alikuwa kwenye maziko ya Marehemu Mhe Balozi Paul James Ndobho.
Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya Musoma Vijijini leo September 14, 2019 imemtunuku HATI ya HESHIMA Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo.
Ndugu Julius Kambarage Masubo, Mjumbe wa Baraza la Wazazi Taifa kutoka Mkoa wa Mara ndiye aliyekuwa MGENI RASMI wa Baraza la Wazazi Wilaya ya Musoma Vijijini lililokutana leo Kijijini Chumwi
Akikabidhi HATI hiyo, MGENI RASMI amesema, “HATI hii ni Ishara ya kipekee ya kutambua Mchango na Utendaji kazi mzuri na uliotukuka wa Mbunge wa Jimbo katika kuitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2015 – 2020 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.
Mgeni Rasmi huyo aliendelea kusema kwamba, HATI hiyo ni kielelezo cha kutambua MCHANGO MKUBWA wa Mbunge huyo kwenye Chama (CCM) na Jumuiya zake zote.
Ndugu Kambarage Masubo ametoa pongezi nyingi kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Muhongo kwa Uongozi Shirikishi unaowaunganisha Wananchi wa Musoma Vijijini katika kuharakisa Maendeleo Jimboni mwao.
Jimbo hili halina malumbano ya kisiasa wala halina mivutano ya kikabila – Mbunge wa Jimbo wanawaunganisha Wananchi wote kwenye MIRADI ya Maendeleo bila ubaguzi wa aina yo yote ile.
Wengine waliotunukiwa HATI ya HESHIMA na Jumuiya ya Wazazi ni pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma, Mhe Charles Magoma Nyambita pamoja na Diwani wa Kata ya Bukima Mhe January Simula.
Ndugu Kambarage Masubo ameikumbusha Jumuiya ya Wazazi wawe kitu kimoja kuhakikisha Ilani ya Chama cha Mapinduzi inatekelezwa kwa kasi kubwa chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt John Joseph Pombe Magufuli.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Musoma Vijijini, Ndugu Phares Maghubu amesisitiza kuwa Jumuiya ya Wazazi inaendelea kuimarisha mipango yao ya utunzaji wa Mazingira, kuhamasisha uboreshaji wa elimu na kuimarisha nidhamu na maadili kwa Vijana ili kuwa na kizazi chenye maadili mazuri na chenye kujituma katika shughuli za ki-uchumi na maendeleo.
CHAMA CHA MAPINDUZI KATA YA RUSOLI YAMTUNUKU MHE. MBUNGE WA JIMBO HATI YA HESHIMA.
WANANCHI WA KIJIJI CHA KABURABURA NAO WAAMUA KUJENGA ZAHANATI YAO
VIKUNDI VYA WATU WENYE ULEMAVU VYANUFAIKA NA MIKOPO KUTOKA HALMASHAURI NA BMZ
VIJANA WANUFAIKA NA KILIMO CHA BUSTANI KWA KUTUMIA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO
UJENZI, UKAMILISHAJI NA UBORESHAJI WA MAABARA ZA MASOMO YA SAYANSI KWENYE SEKONDARI ZA KATA
WAZAZI WA KATA YA TEGERUKA WAAGA VIJANA WAO KWA ZAWADI YA KIPEKEE
MIRADI MIKUBWA YA MAJI INAYOTEKELEZWA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJI
VIJIJI VIWILI VYA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI VYAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAO
SHULE YA MSINGI MURANGI – SOMO LA STADI ZA KAZI LATUMIKA KUIMARISHA KILIMO CHA UMWAGILIAJI
BOMBA LA MAJI SAFI NA SALAMA – MRADI WA MUGANGO-KIABAKARI-BUTIAMA
MIRADI YA SEKTA YA AFYA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

baadhi ya MAJENGO ya Hospitali ya Wilaya inayojengwa Jimboni mwetu (Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti). DC, DED, MADIWANI na Wafanyakazi wa Halmashauri yetu WAPEWE PONGEZI nyingi sana kwa usimamiaji mzuri wa ujenzi wa Hospitali hii
Jimbo lina Kata 21, Vijiji 68, Vitongoji 374
ZAHANATI
* 24 za Serikali zinazotoa huduma
* 4 za Binafsi zinatoa huduma
* 13 MPYA zimeanza kujengwa na Wanavijiji wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
VITUO VYA AFYA
* 2 vya Serikali vinavyotoa huduma za Afya (Murangi & Mugango)
* 1 KIPYA kimeanza kujengwa na Wanavijiji (Kata ya Nyambono) wakishirikiana na Wadau wa Maendeleo yao
HOSPITALI YA WILAYA
* Inajengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti
* Serikali imetoa Tsh 1.5 bilioni kuanza ujenzi wake
* Kila Kijiji kimekubali kuchangia Tsh Milioni 2.
* Mbunge wa Jimbo amekubali kuchangia
ZAHANATI ZINAZOJENGWA NA WANAVIJIJI
(1) Kitongoji cha Burungu, Kijijini Bukumi, Kata ya Bukumi
(2) Kijijini Butata, Kata ya Bukima
(3) Kijijini Chimati, Kata ya Makojo
(4) Kijijini Chirorwe, Kata ya Suguti
(5) Kijijini Kakisheri, Kata ya Nyakatende
(6) Kijijini Kurwaki, Kata ya Mugango
(7) Kijijini Maneke, Kata ya Busambara
(8) Kijijini Mkirira, Kata ya Nyegina
(9) Kijijini Kurukerege, Kata ya Nyegina
(10) Kijijini Nyegina, Kata ya Nyegina
(11) Kijijini Mmahare, Kata ya Etaro
(12) Kijijini Bwai Kwitururu, Kata ya Kiriba
(13) Kijijini Nyasaungu, Kata ya Ifulifu





































































































































































































