MRADI WA UFUNGAJI WA MINARA MIPYA YA MAWASILIANO WAANZA KUTEKELEZWA JIMBONI MWETU

Maombi yetu ya kuomba kuboreshewa mawasiliano ya simu, intaneti, n.k. yaanza kutekelezwa.

Mnara mpya wa VODA umejengwa Kijijini Masinono ndani ya eneo la Bugwema Sekondari. Wanakijiji wanakiri kwamba mawasiliano kupitia mtandao wa VODA kwa sasa ni mazuri sana.

Mbunge wa Jimbo anaendelea kufuatilia maombi yetu ya kuongezewa idadi ya minara ya mawasiliano vijijini mwetu.

Picha ya hapa inaonesha:
Mnara mpya wa VODA uliojengwa ndani ya eneo la Bugwema Sekondari, Kijijini Masinono.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Alhamisi, 14.3.2024