Pamoja na sheria mama za nchi, uongozi wa jimbo la Musoma Vijijini unawakumbusha wanachi kuzingatia sheria na kanuni zifuatazo.

  1. Kila mzazi au mlezi mwenye mtoto aliyefikisha umri wa kuanza shule analazimika kumuandikisha mtoto huyo kuanza shule.
  2. Kila mwananchi anayejishughulisha na shughuli za uvuvi wa samaki, anapaswa kuzingatia kutotumia au kushiriki kwa namna yoyote ile katika uvuvi haramu.
  3. Kila kaya inapaswa kuhakikisha kuwa eneo la kaya husika ni safi.