KIJIJI CHA KABURABURA KIMEANZA KUJENGA ZAHANATI YAKE – TUWAUNGE MKONO

Wiki jana, uamuzi wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kaburabura ulifanywa na wanakijiji wenyewe.

Kamati ya ujenzi iliundwa, na sasa kazi zimeanza kwa kutumia nguvukazi za wanakijiji wenyewe - angalia picha.

Tafadhali tuwaunge mkono kwa kuchangia ujenzi wa Zahanati ya Wana-Kaburabura

Tafadhali tuma mchango wako kwenye Akaunti ya Kijiji chao:

Benki: NMB
Akaunti Na: 30302300684
Jina: Kijiji cha Kaburabura

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Jumanne, 19.3.2024