JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI: VITABU VINAVYOELEZEA UTEKELEZAJI YA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM (2020-2025) VINASAMBAZWA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea vitabu kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo.

Bungeni:
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, amemkabidhi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa vitabu viwili (2) vinavyoelezea miradi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025, ndani ya Jimbo letu.

Mbunge huyo anaendelea kuchapisha vitabu vingine hadi mwaka ujao, 2025.

Tovuti ya Jimbo letu:
www.musomavijijini.or.tz

inazo taarifa muhimu za maendeleo ya Jimbo la Musoma Vijijini. Vitabu hivyo navyo viko kwenye Tovuti hiyo.

Pichani:
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea vitabu kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo.

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Ijumaa, 16.2.2024