UGAWAJI WA VITABU VINAVYOELEZEA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM (2020-2025) UMEANZA

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo ameanza kugawa VITABU VIWILI (Volumes III & IV) vya utekelezaji wa Ilani yetu ya sasa (2020-2025)

Vitabu hivi kama vile viwili (Volumes I & II) vya Ilani ya 2015-2020, vinataja majina ya wachangiaji wa miradi inayotekelezwa Jimboni mwetu.

*Chama Mkoa: wamepewa
*Serikali Mkoa: wamepewa

Ugawaji unaendelea, utafika hadi kwenye Vitongoji. Uchapishaji wa vitabu vipya unaendelea (Volumes IV & V) - Miradi ya maendeleo ya wananchi wa Musoma Vijijini ni mingi!

Wiki ijayo Vitabu 2 (Volumes III & IV) vitawekwa kwenye Tovuti ya Jimbo:
www.musomavijijini.or.tz

Tembelea Tovuti hiyo ya Jimbo letu usome vitabu hivyo na vile vya awali (Volumes I & II, Ilani ya 2015-2020)

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Tarehe:
Ijumaa, 19.1.2024