MAJI YA ZIWA VICTORIA: VIJIJI VINGINE VITATU VYAPATA MAJI YA BOMBA

Vijiji vya Bukumi, Buraga na Busekera vimeanza kutumia Maji SAFI & SALAMA

MWAKA MPYA na CHANZO KIPYA CHA MAJI – Vijiji vya Bukumi, Buraga na Busekera vimeanza kutumia Maji SAFI & SALAMA baada ya Mradi wao wa Maji kukamilika.
RUWASA inaendelea kutekeleza kwa mafanikio makubwa MIRADI ya USAMBAZAJI MAJI vijijini mwetu.
WASIKILIZE (“CLIP” hapa) WANAVIJIJI na VIONGOZI wao wakitoa SHUKRANI zao za dhati kwa SERIKALI yao.
MAJI NI UHAI
MAJI NI UCHUMI
MAJI NI MAENDELEO
Taarifa kutoka:
*Ofisi ya RUWASA
Musoma DC
*Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
1.1.2022