MAKTABA NA MAABARA ZAENDELEA KUJENGWA

MAKTABA ya Shule ya Msingi Karubugu, Kijijini Kurwaki IMEKAMILIKA

MAKTABA ya Shule ya Msingi Karubugu, Kijijini Kurwaki IMEKAMILIKA
MICHANGO YA UJENZI WA MAKTABA HIYO
*Wanakijiji wamechangia nguvukazi na fedha taslimu. Daftari linaloonyesha MICHANGO iliyotolewa liko kwenye Serikali ya Kijiji cha Kurwaki.
*WANAFUNZI na WAKAZI wengine wa Vijiji vya Kurwaki na Kiriba, na Viongozi wa Kata zao WANAISHUKURU sana PCI TANZANIA na MBUNGE wao wa Jimbo Prof Muhongo kwa KUTOA MICHANGO MIKUBWA kukamilisha UJENZI wa MAKTABA ya Shule yao ya Msingi.
Wanafunzi wa S/M Karubugu wanatoka Vijiji vya Kurwaki (Kata ya Mugango) na Kiriba (Kata ya Kiriba)
VITABU vya MAKTABA hiyo vimetolewa na PCI TANZANIA na MBUNGE wao Prof Sospeter Muhongo.
Mbunge huyo ataongenezea VITABU kwenye Maktaba hiyo.
MATUMIZI ya MAKTABA ILIYOJENGWA & KUKAMILIKA
*Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari wanakaribishwa
*Walimu wa shule za Msingi na Sekondari wanakaribishwa.
*Wakazi wa Vijiji na Kata za jirani wanakaribishwa.
UJENZI WA MAKTABA NA MAABARA ZA SAYANSI KWENYE SHULE ZA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI UNAENDELEA.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini