WANAVIJIJI WASHIRIKIANA NA SERIKALI KUTATUA TATIZO LA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA MASHULENI

ukamilishaji wa ujenzi wa Vyumba vipya vya Madarasa vya S/M NYASAUNGU iliyoko Kijijini Nyasaungu, Kata ya Ifulifu.

Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
JIMBO la Musoma Vijijini laendelea kuongoza kwenye UTEKELEZAJI wa ILANI za UCHAGUZI za CCM (2020-2025 & 2015-2020)
MATATIZO YA UPUNGUFU WA VYUMBA VYA MADARASA
SHULE ZA MSINGI
*Vyumba vipya 380 vimejengwa na kukamilika
*Maboma 50 ya Vyumba vipya vya Madarasa yanakamilishwa ujenzi
SHULE ZA SEKONDARI
*Vyumba vipya 78 vya Madarasa vimejengwa na kukamilika
*Maboma 25 ya Vyumba vipya vya Madarasa yanakamilishwa ujenzi
SHULE ya MSINGI NYASAUNGU
KIJIJI cha Nyasaungu ni kimoja kati ya Vijiji 3 (Kabegi, Kiemba na Nyasaungu) vya Kata ya IFULIFU
KIJIJI cha Nyausungu chenye VITONGOJI vitano (5) kina WAKAZI wapatao 315, na kina Shule moja ya Msingi ijulikanayo kwa jina la SHULE ya MSINGI NYASAUNGU
KAIMU MWALIMU MKUU wa Shule hii,  Mwl Stephen  Musibha ameeleza yafuatayo kuhusu Shule hiyo:
*Ilianzishwa Mwaka 1999 na kwa sasa inao Wanafunzi 788
*Mahitaji ya vyumba vya Madarasa ni 14, vilivyopo ni 8
*Darasa la Tatu ndilo lenye MRUNDIKANO mkubwa wa WANAFUNZI darasani, Wanafunzi 131 wanasomea kwenye chumba kimoja cha Darasa.
*Matundu ya Vyoo yanayohitajika ni 39, yapo 8 tu.
*Mahitaji ya Walimu ni 15, waliopo ni 5 tu
*Nyumba 15 za Walimu zinahitajika, zipo 5 za Walimu watano (5) waliopo
MICHANGO YA UJENZI WA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA VYA S/M NYASAUNGU
MWENYEKITI wa Serikali ya Kijiji cha Nyasaungu, Ndugu Magesa Chacha Marera amebainisha MICHANGO inayoendelea kutolewa kama ifuatavyo:
*WANAKIJIJI
(i) NGUVUKAZI za kusomba mawe, kokoto, mchanga na maji ya kujengea
(ii) Kila Kitongoji kinachangia Tsh 107,000 au Matofali 40 kwa kila awamu ya ujenzi
*SERIKALI, kupitia Mradi wake wa EP4R, imechangia  SHILINGI MILIONI 12  kupaua Chumba kimoja cha Darasa na Ofisi moja ya Walimu. Shukrani nyingi kwa SERIKALI yetu.
MICHANGO MINGINE ILIYOTOLEWA KWENYE S/M NYASAUNGU
*PCI Tanzania
imejenga Matundu 8 ya Vyoo vya Wanafunzi. Shukrani nyingi sana kwa PCI Tanzania.
*PCI Tanzania inachimba Kisima cha Maji cha S/M Nyasaungu. Ahsanteni sana PCI Tanzania.
*MBUNGE wa JIMBO
Prof Sospeter Muhongo amechangia:
(i) Saruji Mifuko 50
(ii) Madawati 130
(iii) Vitabu zaidi ya 1,000 vya Maktaba
*MFUKO wa JIMBO
(i) Mabati 108
MATOKEO YA MITIHANI YA TAIFA YA S/M NYASAUNGU
DARASA LA IV (2020)
*Watahiniwa: 92
*Waliofaulu: 92
DARASA LA VII (2020)
*Watahiniwa: 40
*Waliofaulu: 31
OMBI KUTOKA KIJIJINI NYASAUNGU
*KIJIJI hiki kinayo MIRADI mikuu mitatu (3) inayotekelezwa kwa sasa. MIRADI hiyo ni ya ujenzi wa SEKONDARI ya Kijiji, ZAHANATI ya Kijiji na VYUMBA VIPYA vya Madarasa kwenye Shule yao ya Msingi.
*WAZALIWA wa Kijiji cha Nyasaungu wanaombwa kujitokeza kuchangia MAENDELEO ya Kijijini KWAO. WADAU wa MAENDELEO nao wanakaribishwa.
Karibuni sana tuchangie MAENDELEO ya Kijiji cha NYASAUNGU.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini