FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO ZACHANGIA UKAMILISHAJI WA MIUNDOMBINU YA SHULE  ZA MUSOMA VIJIJINI

baadhi ya MIUNDOMBINU inayojengwa kwenye SEKONDARI MPYA ya VIJIJI 2 (Kakisheri & Kigera) vya Kata ya Nyakatende. SEKONDARI hii itafunguliwa Mwezi huu, Januari 2021.

UJENZI na UBORESHAJI wa MIUNDOMBINU ya SHULE zote za Jimboni mwetu unachangiwa na:
* Wanavijiji
* Serikali
* Mbunge wa Jimbo
* Wadau wa Maendeleo, k.m. PCI Tanzania, na Benki za NMB, CRDB na TPB
* Wazaliwa wa baadhi ya Vijiji
IDADI YA SHULE NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
(Jimbo lina Vijiji 68, Kata 21)
(i) SHULE SHIKIZI: 12
Ujenzi na upanuzi wa Shule hizi unaendelea. Baadhi ya Shule hizo tayari zinatoa ELIMU ya AWALI ya WATOTO wa chini ya MIAKA 6.
(ii) SHULE ZA MSINGI: 111
Vyumba vipya vya Madarasa  vinaendelea kujengwa na kuboreshwa kwenye Shule hizi.
Vyumba VIPYA 380 vimejengwa kwenye Shule hizi ndani ya miaka mitano (2016-2020).
MAKTABA zinaendelewa kujengwa (nyingine tayari zimekamilika na zinatumika) kwenye baadhi ya Shule hizi
MIUNDOMBINU mingine inaendelea kujengwa na kuboreshwa, hasa NYUMBA mpya za WALIMU na VYOO vipya.
(iii) SHULE ZA MSINGI ZA BINAFSI: 3
*Zipo Shule za Binafsi 3 ndani ya Jimbo letu.
(iv) SEKONDARI ZA KATA:
20 + 5 mpya
SEKONDARI MPYA zilizofunguliwa Mwaka jana (2020) ni mbili:
 * Dan Mapigano Memorial Secondary School ya Kata ya Bugoji
* Busambara Secondary School ya Kata ya Busambara
Vyumba VIPYA 120 vimejengwa kwenye Sekondari zetu 20 ndani ya miaka mitano (2016-2020).
(v) SEKONDARI
 ZA BINAFSI: 2
* Zipo Sekondari 2 za Madhehebu ya Dini ya Katoliki (RC) na Wasabato (SDA)
(vi) SEKONDARI MPYA ZA KATA ZINAZOJENGWA
SEKONDARI zinazojengwa na zitakazofunguliwa Mwaka huu (2021) ni:
* Seka Secondary School ya Kata ya Nyamrandirira (Sekondari ya pili ya Kata)
* Nyasaungu Secondary School ya Kata ya Ifulifu (Sekondari ya kwanza ya Kata)
* Kigera Secondary School, Kata ya Nyakatende (Sekondari ya pili ya Kata)
* Bukwaya Secondary School ya Kata ya Nyegina inakamilisha miundombinu (Sekondari ya pili ya Kata)
* Ifulifu Secondary School ya Kata ya Ifulifu inayojengwa Kijijini Kabegi. Inakamilisha miundombinu (Sekondari ya Kata ya pili)
USIMAMIAJI MZURI & MADHUBUTI
*MKUU wa Wilaya (DC), Dr Vicent Anney Naano anapongezwa sana kwa KUSIMAMIA ujenzi huu na mwingine, kwa MAFANIKIO makubwa, tokea Mwaka 2016.
* HALMASHAURI yetu chini ya Mkurugenzi (DED) John Lipesi Kayombo inafanya kazi vizuri.
MGAO WA FEDHA ZA
MFUKO WA JIMBO
(Jan 2021, Tshs 52.43M)
MANUNUZI & UGAWAJI:
*Mabati: 1,134
*Saruji Mifuko (supa):1,020
JUMLA: Tshs 52,176,378 (Tshs 52.18M)
* HALMASHAURI yetu ndiyo inayotunza FEDHA za MFUKO wa JIMBO, na ndiyo inafanya MANUNUZI ya VIFAA vya UJENZI baada ya kupewa MAELEKEZO kutoka kwenye Kamati ya Mfuko wa Jimbo chini ya Mwenyekiti wake, Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo
MGAO – MALENGO
* Kukamilisha MIUNDOMBINU ya SHULE MPYA ili zifunguliwe Mwaka huu (2021).
* Kuongeza idadi ya Vyumba VIPYA vya Madarasa kwenye Sekondari zilizofunguliwa Mwaka jana (2020)
SEKONDARI MPYA (2021):
(1) SEKA SECONDARY SCHOOL
(Kata ya Nyamrandirira)
* Mabati 216
* Saruji Mifuko 200
(2) KIGERA SECONDARY SCHOOL
(Kata ya Nyakatende)
* Mabati 216
* Saruji Mifuko 200
(3) NYASAUNGU SECONDARY SCHOOL
(Kata ya Ifulifu)
* Mabati 54
* Saruji Mifuko 80
SEKONDARI MPYA ZA MWAKA JANA (2020)
(4) DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL
(Kata ya Bugoji)
* Mabati 216
* Saruji Mifuko 180
(5) BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL
(Kata ya Busambara)
* Mabati 216
* Saruji Mifuko 180
SHULE ZA MSINGI MPYA
(6) MWIKOKO SHULE SHIKIZI
(Kitongoji cha Mwikoko, Kijiji cha Chitare, Kata ya Makojo)
* Mabati 108
* Saruji Mifuko 80
(7) NYASAENGE SHULE SHIKIZI
(Kitongoji cha Nyasaenge, Kijiji cha Kataryo, Kata ya Nyakatende)
* Mabati 108
* Saruji Mifuko 100
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini