WANAVIJIJI WA KATA YA NYEGINA WAAINISHA VIPAUMBELE VYAO VYA UTEKELEZAJI WA ILANI MPYA YA CCM

MIKUTANO ya KAMPENI za CCM ndani ya Kata ya Nyegina.

Alhamisi, 15.10.2020, MGOMBEA UBUNGE wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO, amefanya MIKUTANO 3 ya KAMPENI za CCM ndani ya Kata ya Nyegina.
MIKUTANO 3 imefanywa kwenye VIJIJI vya Kurukerege, Nyegina na Mkirira.
WANAVIJIJI wa Kata hii wamesema KURA ZOTE watazipeleka CCM kwenye nafasi ya URAIS, UBUNGE na UDIWANI.
WANAVIJIJI wameamua hivyo baada ya kuvutiwa na ILANI MPYA YA CCM ya 2020-2025 na VIPAUMBELE vyao vya MAENDELEO vimo ndani ya ILANI hii.
*VITENDO KWANZA
*MAENDELEO KWANZA
VIPAUMBELE VYA KIJIJI CHA KURUKEREGE
* Kukamilisha ujenzi wa ZAHANATI ya Kijiji chao
* Kukamilisha ujenzi wa Vyumba Vipya vya Madarasa vya SHULE ya MSINGI BUKWAYA ambayo ni mpya yenye Madarasa 5.
VIPAUMBELE VYA KIJIJI CHA NYEGINA
* Kukamilisha WODI ya Mama & Mtoto inayojengwa kwenye ZAHANATI ya Nyegina.
VIPAUMBELE VYA KIJIJI CHA MKIRIRA
* Kukamilisha ZAHANATI ya Kijiji chao
VIPAUMBELE VYA KATA (Vijiji vyote 3)
* ELIMU: Kukamilisha ujenzi wa SEKONDARI ya PILI (Bukwaya Secondary School) itakayofunguliwa Januari 2021. Inajengwa Kijijini Nyegina
* MAJI VIJIJINI: Kata iko kwenye MIRADI 2 ya MAJI kutoka Ziwa Victoria –
(i) MAJI ya MUWASA
Maji ya Mji wa Musoma YAMEANZA kusambazwa kwenye VIJIJI jirani na Mji huo vikiwemo VIJIJI vyote vya Kata za Etaro, Nyegina, Nyakatende na Ifulifu.
(ii) MRADI wa MAZIWA MAKUU
* Vijiji vyote 3 vya Kata hii ni miongoni mwa VIJIJI 33 vya Jimboni mwetu vilivyoko kwenye Mradi huu.
* UMEME VIJIJINI: Baadhi ya Vitongoji vya Vijiji vyote 3 vimeishapatiwa umeme na USAMBAZAJI unaendelea hadi kukamilisha upelekaji wa UMEME kwenye Vitongoji vyote.
UTAMADUNI, MICHEZO NA SANAA
* ILANI mpya ya CCM ya 2020-2025 inaeleza umuhimu wa Utamaduni, Michezo na Sanaa kwa TAIFA letu
*Jimbo letu LINAENDELEA kustawisha ukuaji na uimarikaji wa KWAYA na  NGOMA zetu za ASILI.
MICHANGO ya PROF MUHONGO kwenye MIRADI yote ya MAENDELEO ya Kata hii inatambuliwa na kutolewa shukrani nyingi.
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
15 Oktoba 2020