KAMPENI ZA CCM – PROF MUHONGO ARUDI VIJIJINI KUSISITIZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO YA CHAGUO LAO 

Jumamosi, 24.10.2020, MGOMBEA UBUNGE wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO amerudi kwenye Kata ya MAKOJO na kupiga KAMPENI kwenye Vijiji vya CHITARE na CHIMATI.
UTEKELEZAJI WA ILANI MPYA YA CCM (2020-2025) NDANI YA KATA YA MAKOJO
(1) MAJI VIJIJINI
* Miradi wa MAJI kutoka ZIWA VICTORIA unatekelezwa ndani ya Kata hii – kukamilisha Mradi wa Bomba la Maji la Chitare-Makojo na baadae kusambaza Maji ya Bomba hili hadi Kijiji cha Chimati
(2) UMEME VIJIJINI
*Vijiji vyote 3 vya Kata hii (Chimati, Chitare & Makojo) vinayo MIUNDOMBINU ya usambazaji wa UMEME, na baadhi ya Vitongoji vyake tayari vimepewa UMEME wa REA. Vitongoji vilivyosalia vitapewa UMEME, kama ilivyoelezwa ndani ya ILANI ya UCHAGUZI ya CCM (2020-2025)
VIPAUMBELE VYA KILA KIJIJI
(1) KIJIJI CHA CHIMATI
*Kukamilisha ujenzi wa ZAHANATI ya Kijiji chao
*Kujenga SEKONDARI ya Kijiji chao kwani SEKONDARI ya Kata iko mbali Kijijini Makojo.
(2) KIJIJI CHA CHITARE
*Kujenga SEKONDARI ya Kijiji chao kwani SEKONDARI ya Kata iko mbali Kijijini Makojo
*WADI ya MAMA & MTOTO kujengwa kwenye ZAHANATI yao
(3) KIJIJI CHA MAKOJO
*Kujenga ZAHANATI ya Kijiji chao
*VITENDO KWANZA
*MAENDELEO KWANZA
KATA YA MAKOJO imeahidi KUTOA KURA ZOTE kwa CCM – sababu – ILANI ya UCHAGUZI ya CCM (2020-2025) ina VIPAUMBELE vya MIRADI ya MAENDELEO yao
VIAMBATANISHO – Matukio ya leo ya KAMPENI za CCM kwenye Kijiji cha Chimati, Kata ya Makojo
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
24.10.2020