MIRADI YA MAENDELEO YAING’ARISHA CCM NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

WanaMusoma Vijijini wakisikiliza kwa makini Katika mkutano mmojawapo wa Kampeni.

MALENGO ya KAMPENI za CCM ndani ya Vijiji 68 vya Jimbo la Musoma Vijijini ni MAENDELEO (kwa ujumla wake) & USTAWI wa JAMII. Hivyo, USHINDI wa kishindo kizito.
WANANCHI wa kila KIJIJI na kila KATA, kwa kutumia ILANI ya UCHAGUZI ya CCM (2020-2025), wanabainisha VIPAUMBELE vyake vya MIRADI ya MAENDELEO.
KATA YA BUSAMBARA
Kata hii ina VIJIJI 3 (Kwikuba, Maneke na Mwiringo) na VIPAUMBELE vyake ni:
(1) ELIMU & MAFUNZO
Kata ya Busambara inayo SEKONDARI MPYA (Busambara Secondary School) iliyofunguliwa Januari 2020.
Ujenzi wa Vyumba vipya vya Madarasa, Maabara, Maktaba, Nyumba za Walimu, n.k. unaendelea.
MICHANGO ya ujenzi wa SEKONDARI hii inatolewa na WANANCHI, SERIKALI, PROF MUHONGO na WAZALIWA wa Kata hii.
(2) MAJI VIJIJINI
 MIRADI 2 ya MAJI ya kutoka Ziwa Victoria itatekelezwa ndani ya Kata hii:
 (i) Vijiji vyote vitatu vimo ndani ya Mradi wa Maziwa Makuu
(ii) Vijiji vyote vitatu vimo ndani ya Mradi wa Mugango-Kiabakari- Butiama.
(3) UMEME VIJIJINI
Vijiji vyote vitatu vinayo miundombinu ya umeme na baadhi ya Vitongoji vimeishapatiwa umeme. Vitongoji vilivyosalia navyo vitapewa umeme kama inavyoelezwa ndani ya ILANI ya CCM ya 2020-2025
KIJIJI CHA MWIRINGO
* Kukamilisha ujenzi wa SHULE SHIKIZI iliyoko Kitongoji cha Ziwa. Shule itapanuliwa hadi  kufikia Darasa la VII (Shule ya Msingi kamili).
KIJIJI CHA KWIKUBA
* Nyumba za Wafanyakazi wa ZAHANATI yao.
KIJIJI CHA MANEKE
* Kukamilisha ujenzi wa ZAHANATI ya Kijiji chao
UTEKELEZAJI wa MIRADI hiyo hapo juu unaanza tarehe 1.11.2020
WANANCHI wa Kata ya BUSAMBARA wanasema KURA ZOTE watapewa WAGOMBEA WATATU wa CCM (Urais, Ubunge na Udiwani)
*VITENDO KWANZA
*MAENDELEO KWANZA
VIAMBATANISHO (Picha hapo juu) ni Kampeni za CCM ndani ya Kata ya Usambara.
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
14.10.2020