KAMPENI ZA CCM NI ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO: KATA YA NYAKATENDE INAYO MIRADI 5 YA KIPAUMBELE

Jumatatu, 12.10.2020 MGOMBEA UBUNGE wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO amefanya KAMPENI 3 na kukamilisha UOMBAJI wa KURA kwenye VIJIJI vyote 4 vya Kata ya Nyakatende (Kakisheri, Kamuguruki, Kigera na Nyakatende).
MIRADI yote ya KIPAUMBELE ya Kata ya Nyakatende CHIMBUKO LAKE ni ILANI za CCM za 2015-2020 na 2020-2025
(1) MAJI VIJIJINI
*Vijiji vyote 4 vya Kata hii vitapata MAJI kutoka Ziwa Victoria. Ipo MIRADI 3 ya Ziwa Victoria na unaotekelezwa SASA HIVI ni wa MAJI kutoka MUWASA (Maji ya Mji wa Musoma). SERIKALI ya CCM inatekeleza AHADI yake ya kusambaza MAJI VIJIJINI.
(2) UMEME VIJIJINI
* Vijiji vyote 4 vinayo Miundombinu ya kuendelea na usambazaji wa UMEME VIJIJINI kwenye Vitongoji vilivyosalia.
MIRADI INAYOHITAJI MICHANGO YA WANANCHI & KUTOKA SERIKALINI
(3) ELIMU & MAFUNZO
* SEKONDARI ya PILI (Kigera Secondary School) inajengwa na Vijiji 2 itafunguliwa JANUARI 2021. MICHANGO inatoka kwa Wanavijiji, Wazaliwa wa Vijiji 2 (Kakisheri & Kigera) na Prof Muhongo.
* SHULE SHIKIZI KIHUNDA inajengwa Kijijini Kamuguruki kwa kutumia MICHANGO ya Wananchi na Prof Muhongo
(4) HUDUMA ZA AFYA
* ZAHANATI mpya ya Kijiji cha Kakisheri tayari imeanza kujengwa
* ZAHANATI mpya ya Kijiji cha Kamuguruki itaanza kujengwa baada ya tarehe 28.10.2020
* KITUO cha AFYA cha Kata ya Nyakatende kitajengwa Kijijini Kigera.
KAMPEZI za CCM ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini ni KAMPENI za UTEKELEZAJI wa ILANI MPYA ya CCM ya 2020-2025
WAPIGA KURA WA KATA YA NYAKATENDE wanasema:
*Dkt Magufuli: 100%
*Prof Muhongo: 100%
*Ndugu Kishe: 100%
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Picha hapo juu ni moja kati ya MATUKIO mbalimbali ya KAMPENI 3 za leo za CCM ndani ya Kata ya Nyakatende
*VITENDO KWANZA
* MAENDELEO KWANZA
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
12 Oktoba 2020