KISIWA CHA RUKUBA CHAIKUBALI ILANI MPYA YA CCM NA KUAMUA KUJENGA KITUO CHA AFYA

Kisiwa cha RUKUBA kiko ndani ya Kata ya ETARO yenye VIJIJI 4 (Busamba, Etaro, Mmahare na Rukuba).
Leo, Jumapili, 11.10.2020 MGOMBEA UBUNGE wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO, alifanya MIKUTANO 4 ya KAMPENI za CCM ndani ya Kata hiyo – akianzia Kisiwani RUKUBA.
VIPAUMBELE VIKUU VYA UTEKELEZAJI WA ILANI MPYA YA CCM NDANI YA KATA YA ETARO
(1) MAJI SAFI & SALAMA
* Vijiji vya Mmahare, Etaro na Busamba vinasambaziwa MAJI ya MUWASA (Maji ya Mji wa Musoma kutoka Ziwa Victoria) na tayari uchimbaji wa mitaro na utandikaji wa mabomba umeanza. SERIKALI ya CCM inatekeleza AHADI yake ya USAMBAZAJI wa MAJI VIJIJINI.
* Kisiwa cha RUKUBA kiko kwenye Mradi wa Maziwa Makuu – kutumia Maji ya Ziwa Victoria.
(2) UMEME VIJIJINI
* Kisiwa cha RUKUBA kimeanza kutumia UMEME wa JUA (solar)
* VITONGOJI vya Vijiji 3 vilivyosalia vitapewa UMEME wa REA kama ilivyoainishwa ndani ya ILANI MPYA ya CCM ya 2020-2025.
(3) ELIMU & MAFUNZO
* Kata ya ETARO inayo SEKONDARI MOJA inayotumiwa na Vijiji 4. Haitoshi! SEKONDARI ya PILI ya Kata hiyo itajengwa Kijijini Busamba.
(4) HUDUMA ZA AFYA
* Kisiwa cha RUKUBA kitapanua ZAHANATI yake na kuwa KITUO cha AFYA. WODI ya MAMA & MTOTO inayojengwa Kisiwani hapo kwa kutumia MICHANGO ya WANANCHI & PROF MUHONGO, litakuwa (WODI) sehemu ya KITUO cha AFYA hicho.
* Kijiji cha MMAHARE kitakamilisha ujenzi wa ZAHANATI ya Kijiji chake. WADAU wengi wa MAENDELEO, akiwemo PROF MUHONGO, wanachangia ujenzi wa ZAHANATI hii.
KURA ZA KATA YA ETARO – Wananchi wanasema:
* Dkt Magufuli: 100%
* Prof Muhongo:100%
* Ndg Kigwa: 100%
VIAMBATANISHO vya hapa: matukio mbalimbali ya KAMPENI za CCM ndani ya Kata ya ETARO
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
11 Oktoba 2020