ILANI MPYA YA CCM IMEBEBA VIPAUMBELE VYA MAENDELEO YA KATA YA TEGERUKA

Tarehe 9.10.2020, MGOMBEA UBUNGE wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO, alikuwa na MIKUTANO ya KAMPENI kwenye VIJIJI 2 (Mayani & Tegeruka) vya Kata ya TEGERUKA. Hapo awali alishafanya MKUTANO wa KAMPENI kwenye KIJIJI cha Kataryo.
VIPAUMBELE vya MAENDELEO ya Vijiji hivyo 3 vya Kata hiyo vimo kwenye ILANI MPYA ya UCHAGUZI ya CCM ya 2020-2025. Kwa hiyo, UTEKELEZAJI unaanza mara moja baada ya UCHAGUZI wa tarehe 28.10.2020.
MAJI KWA VIJIJI VYOTE VYA KATA YA TEGERUKA
* SERIKALI ya CCM inao MRADI wa Tsh BILIONI 70 wa MAJI ya BOMBA ya Ziwa Victoria – Mugango – Kiabakari – Butiama. VIJIJI vyote 3 vya Kata ya TEGERUKA nitapata MAJI kutoka kwenye Bomba hili.
* FEDHA za MRADI huu zimetolewa na Serikali ya Saudi Arabia, BADEA (Khartoum, Sudan) na Serikali yetu. Mradi utaanza Januari 2021 au kabla.
UMEME KWA VIJIJI VYOTE VYA KATA YA TEGERUKA
* Kwa kuwa UMEME tayari unatumiwa na baadhi ya WAKAZI wa VIJIJI 3 vya Kata hii, WANANCHI wana imani kubwa na SERIKALI ya CCM kukamilisha USAMBAZAJI uliosalia – na hili nalo limo ndani ya ILANI MPYA ya CCM.
KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SEKONDARI YA KATA
* Ujenzi wa MAABARA, MAKTABA, n.k  kwenye Tegeruka Sekondari unaendelea.
KIJIJI CHA KATARYO:
WANANCHI wameamua kujenga:
* ZAHANATI ya Kijiji chao
* SHULE SHIKIZI Nyasaenge
VIJIJI VYA MAYANI & KATARYO:
* WANANCHI wameamua kujenga SEKONDARI ya PILI ya Kata itakayojengwa katikati ya Vijiji hivyo viwili. Ujenzi unaanza tarehe 1.11.2020
KAMPENI ZA UCHAGUZI za Jimbo la Musoma Vijijini ni KAMPENI za MATAYARISHO ya UTEKELEZAJI wa ILANI MPYA ya CCM (2020-2025)
* VITENDO KWANZA
* MAENDELEO KWANZA
KURA ZA KATA YA TEGERUKA – Wananchi wamesema:
* Dkt Magufuli: 100%
* Prof Muhongo: 100%
* Ndg Mashauri: 100%
VIAMBATANISHO vya hapa: baadhi ya Matukio ya KAMPENI za UCHAGUZI ndani ya Kata ya Tegeruka.
“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”
Sospeter Muhongo
Jimbo la Musoma Vijijini
10.10.2020