WANANCHI WA KATA YA MUSANJA WATOA VIPAUMBELE VYAO KWA MIAKA 5 YA UTEKELEZAJI WA ILANI MPYA YA CCM (2020-2025)

Ijumaa, tarehe 2.10.2020, KATA ya MUSANJA yenye VIJIJI 3 (Mabui Merafuru, Musanja na Nyabaengere) ilikuwa kwenye KAMPENI za UCHAGUZI za Chama cha Mapinduzi (CCM)

WAGOMBEA UBUNGE (Prof Muhongo) na UDIWANI (Ndugu Mwira) wa CCM walinadi SERA na MIRADI ya MAENDELEO iliyoko kwenye ILANI MPYA (2020-2025) ya Chama chao.

MIKUTANO 2 ya KAMPENI ilifanywa kwenye VIJIJI 2 (Musanja & Mabui Merafuru).

WANANCHI  WALIVUTIWA SANA na SERA za CCM na kuahidi kutoa KURA ZOTE kwa WAGOMBEA wa CCM kwa nafasi ya URAIS (Dkt Magufuli), UBUNGE (Prof Muhongo) na UDIWANI (Ndg Ernest John Mwira).

MIRADI ya KIPAUMBELE ya KATA ya MUSANJA ni:

*Kukamilishwa kwa usambazaji wa UMEME kwenye Vitongoji vilivyosalia

*Kuanza kwa utekelezaji wa Mradi wa MAJI ya kutoka Ziwa Victoria (Chumwi, Kata ya Nyamrandirira) hadi Mabui Merafuru (Kata ya Musanja). Wataalamu walishakamilisha USANIFU wa Mradi huu.

*Ukamilishaji wa ujenzi wa SHULE Shikizi Gomora na kuipanua iwe Shule ya Msingi inayojitegemea.

*Kujenga ZAHANATI 1 kwenye Kijiji 1 kati ya Vijiji 3. Kwa sasa Kata ya Musanja inatumia Kituo cha Afya ya Murangi.

*SEKONDARI kwenye Kijiji cha Musanja ambacho kiko mbali na Sekondari ya Kata iliyoko Kijiji cha Mabui Merafuru

*VITENDO KWANZA

*MAENDELEO KWANZA

VIAMBATANISHO vya hapa:

*Kwaya ya Musanja

*Matukio mengine ya Kampeni

“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE KWA PAMOJA”

Sospeter Muhongo

Jimbo la Musoma Vijijini

3 Oktoba 2020