MIRADI YA UJENZI WA SEKONDARI MPYA TISA (9) ZA KATA ITAKAMILISHWA NA WANANCHI WAKISHIRIKIANA NA SERIKALI YA CCM

 

Jimbo la Musoma Vijijini lina JUMLA ya SEKONDARI 20 za KATA. Sekondari zote hizi ziko kwenye UJENZI wa MAABARA, MAKTABA, VYUMBA VIPYA VYA MADARASA, OFISI & NYUMBA ZA WALIMU, n.k.

Jimbo la Musoma Vijijini lina UJENZI wa SEKONDARI MPYA TANO (5) za Kata zilizopangwa zifunguliwe mwakani (Januari 2021). SEKONDARI MPYA hizo ni:

(i) Kigera, Kata ya Nyakatende,

(ii) Nyasaungu, Kata ya Ifulifu,

(iii) Ifulifu (inajengwa Kijijini Kabegi), Kata ya Ifulifu,

(iv) Seka, Kata ya Nyamrandirira, na

(v) Bukwaya, Kata ya Nyegina.

Kata hizo 5 zitakuwa na SEKONDARI zaidi ya MOJA ndani ya Kata zao.

*VITENDO KWANZA*

Kata nyingine za Jimbo la Musoma Vijijini nazo zimepanga kuwa na SEKONDARI zaidi ya MOJA ndani ya Kata zao. Kwa hiyo, zimeishafanya maamuzi ya kuanza kujenga SEKONDARI MPYA. Kata hizo ni:

(vi) Suguti, itajenga Sekondari mpya Kijijini Wanyere,

(vii) Tegeruka, Sekondari mpya itajengwa katikati ya Vijiji vya Kataryo na Mayani,

(viii) Etaro, itajenga Sekondari mpya Kijijini Busamba, na

(ix) Mugango, Sekondari mpya itajengwa katikati ya Vijiji vya Kurwaki na Nyang’oma

Ifikapo MWAKA 2025, Jimbo la Musoma Vijijini, lenye Kata 21 litakuwa na:

* SEKONDARI 29 za Kata (Serikali)

* SEKONDARI 2 za Binafsi (SDA & KATOLIKI)

* VETA 1 – maombi yameishapelekwa Serikalini

*MAENDELEO KWANZA*

*CHAGUENI CCM  TUKAMILISHE MIRADI YETU

*CHAGUENI DKT MAGUFULI ili TUKAMILISHE MIRADI YETU*

* CHAGUENI PROF MUHONGO & MADIWANI 21 WA CCM wa KATA 21 za Jimbo letu ili TUKAMILISHE MIRADI YETU

PICHA zilizopo hapa zinaonesha ujenzi unaoendelea kwa baadhi ya SEKONDARI MPYA za KATA za Jimbo la Musoma Vijijini.

“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA”

Sospeter Muhongo

Jimbo la Musoma Vijijini

29 Sept 2020