SHULE MPYA 11 ZA MSINGI KUKAMILISHWA NDANI YA MIAKA 5 (2020-2025) – CHAGUA CCM, CHAGUA DKT MAGUFULI MIRADI IKAMILIKE

 

MWAKA jana (2019) SHULE za MSINGI za  Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC), yenye Jimbo la Musoma Vijijini, ziliongoza (NAMBA MOJA) Mkoa wa Mara kwenye MITIHANI ya Darasa la Nne (Std IV).

WANANCHI wa VIJIJI 11 ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini WAMEAMUA kujenga SHULE MPYA 11 za MSINGI kwa madhumuni ya kuongeza UBORA wa ELIMU itolewayo kwenye SHULE za MSINGI za maeneo yao.

Baadhi ya WANAFUNZI wa Shule za Msingi wanatembea umbali mrefu (kati ya kilomita 2 na 5) kwenda masomoni, na kwenye baadhi ya SHULE za MSINGI kuna MIRUNDIKANO mikubwa MADARASANI.

Kwa hiyo, WANANCHI, kwa kutumia NGUVUKAZI zao na kwa KUSHIRIKIANA na SERIKALI ya CCM, wameamua kutatua matatizo haya!

SHULE SHIKIZI 11 zinajengwa kwenye VIJIJI 11 vya Jimbo hili. Baadhi ya SHULE hizi tayari zina MADARASA ya AWALI na zimeanza kutoa MASOMO ya Darasa la Kwanza na Pili (Std I & II).

Ndani ya MIAKA 5 ya UTEKELEZAJI wa ILANI ya CCM (2020-2025), SHULE hizi 11 zitaendelea kujengwa na kukamilishwa, yaani kuwa SHULE za MSINGI kamili.

*CHAGUA CCM,

*CHAGUA MAENDELEO KWA VITENDO

ORODHA YA SHULE SHIKIZI ZINAZOJENGWA:

(1) Binyango: Kijijini Kabegi, Kata ya Ifulifu

(2) Buanga: Kijijini Buanga, Kata ya Rusoli

(3) Buraga Mwaloni: Kijijini Buraga, Kata ya Bukumi

(4) Egenge: Kijijini Busamba, Kata ya Etaro

(5) Gomora: Kijijini Musanja, Kata ya Musanja

(6) Kaguru: Kijijini Bugwema, Kata ya Bugwema

(7)  Karusenyi: Kijijini Mikuyu, Kata ya Nyamradirira

(8) Rwanga: Kijijini Kasoma, Kata ya Nyamradirira

(9) Mwikoko: Kijijini Chitare, Kata ya Makojo

(10) Kihunda: Kijijini Kamguruki, Kata ya Nyakatende

(11) Ziwa: Kijijini Mwiringo, Kata ya Busambara

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, PROF MUHONGO ni sehemu ya MAFANIKIO ya UJENZI wa SHULE SHIKIZI hizi. Baada ya UCHAGUZI ataendelea KUSHIRIKIANA na WANANCHI na SERIKALI ya CCM kukamilisha ujenzi wa SHULE hizi.

PICHA zilizoko hapa zinaonyesha baadhi ya SHULE SHIKIZI zinazojengwa ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.

“TUMETEKELEZA KWA KISHINDO, TUNASONGA MBELE PAMOJA.”

Sospeter Muhongo

Jimbo la Musoma Vijijini

28 Sept 2020