MIRADI YA MAENDELEO YA KATA YA NYAKATENDE ITAKAMILISHWA NA CCM

Kampeni za CCM kwenye Kata ya Nyakatende.

Jumanne, 22.9.2020, WANANCHI wa Kata ya NYAKATENDE waliamua wazi wazi kwamba kwenye Kata yao yenye VIJIJI VINNE (Kakisheri, Kamuguruki, Kigera na Nyakatende) KURA zote zitaenda CCM.
SEKONDARI ya PILI (Kigera Secondary School) inayojengwa Kijijini Kigera imepangwa ifunguliwe mwakani (Januari 2021). MAJENGO muhimu ya awali yanaezekwa na WANANCHI wanayo imani kubwa sana na WAGOMBEA wa CCM wa nafasi za URAIS, UBUNGE na UDIWANI kwamba ndio wenye uwezo na kutoa ushirikiano wa SEKONDARI hiyo mpya ifunguliwe Januari 2021.
KIJIJI cha Kakisheri kinajenga ZAHANATI yake. HALMASHAURI ya Wilaya ya Musoma (Musoma DC) imepanga kujenga KITUO cha AFYA kwenye Kata hiyo kwa kutumia MICHANGO na NGUVUKAZI ya WANANCHI wa Kata hiyo.
WANANCHI wanasema MIRADI hii na mingine ya MAENDELEO (k.m. usambazaji wa MAJI na UMEME) itakamilishwa kwa ushirikiano na SERIKALI ya CCM.
UAMUZI wa KATA ya NYAKATENDE ni huu – “KURA ZOTE kwa MAGUFULI (Urais), MUHONGO (Ubunge) na MARERE (Udiwani).”
*VITENDO KWANZA
*MAENDELEO KWANZA