CHAGUENI CCM NCHI IZIDI KUNG’ARA – SHAIRI KUTOKA KIJIJI CHA KASOMA

WANANCHI wa Kata ya Nyamrandirira yenye VIJIJI 5 wamewaomba Prof SOSPETER MUHONGO (Mgombea Ubunge) na Mwl NYEOJA WANJARA (Mgombea Udiwani) waungane nao tarehe 5 Novemba 2020 kukamilisha MAJENGO ya AWALI yanayohitajika ili SEKA SEKONDARI ifungiliwe Januari 2021.

 

VIJIJI 5 (Chumwi, Kaboni, Kasoma, Mikuyu na Seka) vya Kata ya Nyamrandirira vinayo SEKONDARI MOJA (Kasoma Secondary School) ambayo kwa sasa imeelemewa na WINGI wa WANAFUNZI kutoka kwenye vijiji hivyo. WANAFUNZI wengine wanatembea mwendo wa zaidi ya kilomita 10 kwenda masomoni Kasoma Sekondari.

 

Kwa hiyo, KATA hiyo imeamua kuanza KUTEKELEZA ILANI MPYA YA CCM (2020-2025) kwa KUKAMILISHA UJENZI wa MIUNDOMBINU INAYOHITAJIKA kwa ufunguzi wa SEKONDARI yao mpya (Seka Secondary School) inayojengwa Kijijini Seka.

 

Sospeter Muhongo

Jimbo la Musoma Vijijini

25.9.2020