CCM YAENDELEA KUNG’ARA NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Waziri Mkuu, Mhe Kassim Majaliwa Majaliwa akiteta jambo na Prof Muhongo

Jumatatu, 21.9.2020, Waziri Mkuu, Mhe Kassim Majaliwa MAJALIWA amepiga KAMPENI yenye MAFANIKIO MAKUBWA ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini.
Mhe Waziri Mkuu ameelezea MAFANIKIO MAKUBWA yaliyopatikana kwenye UTEKELEZAJI wa ILANI ya CCM ya 2015-2020 chini ya UONGOZI na USIMAMIZI wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Joseph Pombe MAGUFULI
Mhe Waziri Mkuu ametoa maelezo ya kina juu ya UTEKELEZAJI wa ILANI mpya ya CCM ya 2020-2025 na kuwadhibitishia WANANCHI wa Jimbo la Musoma Vijijini kwamba MIRADI ya MAENDELEO ya Jimbo hilo ITATEKELEZWA na KUKAMILISHWA na SERIKALI ya CCM chini ya UONGOZI wa Mhe Dkt John Joseph Pombe MAGUFULI.
MIRADI ya MAENDELEO ya Jimbo la Musoma Vijijini INAYOTEKELEZWA kwa USHIRIKIANO wa SERIKALI na WANANCHI wa Jimbo hilo ni mingi mno ikiwemo ya ujenzi wa barabara ya lami ya Musoma-Makojo-Busekera, Hospital ya Wilaya, Zahanati mpya na Vituo vya Afya vipya, Sekondari mpya, ukamilishaji wa usambazaji wa MAJI na UMEME vijijini, upanuzi wa kilimo cha umwagiliaji, n.k. MIRADI mipya imo ya ujenzi wa VETA, Makao Makuu ya Halmashauri Kijijini Murangi, n.k.
Waziri Mkuu amekabidhi ILANI ya UCHAGUZI ya CCM ya 2020-2025 kwa Mgombea Ubunge (Prof Muhongo) wa CCM wa Jimbo la Musoma Vijijini.
Prof Muhongo amesema kwamba WANANCHI wa Jimbo la Musoma Vijijini, kwa KUSHIRIKIANA na SERIKALI yao ya CCM, wataanza KUTEKELEZA ILANI mpya ya CCM ya 2020-2025 kuanzia tarehe 1.11.2020. Muhtasari wa MIRADI ya Jimbo hilo imekabidhiwa kwa Mhe Waziri Mkuu.
Mhe Waziri Mkuu ameshuhudia UTAYARI na MWITIKIO mkubwa wa WANANCHI wa Jimbo la Musoma Vijijini wa KUTOA KURA NYINGI SANA kwa MGOMBEA URAIS wa CCM, Mhe Dkt John Joseph Pombe MAGUFULI.
SHUKRANI nyingi zimetolewa kwa WAZIRI MKUU, Mhe Kassim Majaliwa MAJALIWA kwa kuwahutubia WANANCHI Kijijini Bukima, Kijijini Suguti (Kusenyi), Kijijini Kwikuba, Kijijini Mugango na Kijijini Mkirira. AMEFANIKIWA SANA kuwaombea KURA WAGOMBEA wa CCM wa nafasi za URAIS, UBUNGE na UDIWANI.
WANANCHI wa JIMBO la Musoma Vijijini WAMEAHIDI kupiga kura, bila kukosa, tarehe 28.10.2020 na kupata USHINDI MKUBWA MNO MNO kwa CHAMA cha MAPINDUZI (CCM).
Sospeter Muhongo
21 Sept 2020