JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI – USAMBAZAJI WA MABANGO,  VIPEPERUSHI & VITABU VYA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA ILANI ILIYOPITA

usambazaji wa MABANGO & VIPEPERUSHI ndani ya Vijiji vyote 68 vya Jimbo la Musoma Vijijini.

(1) MABANGO 4,000 (elfu nne) ya MGOMBEA URAIS wa CCM, Mhe Rais Dkt John Joseph Pombe MAGUFULI yanasambazwa ndani ya Vijiji vyote 68.
(2) VIPEPERUSHI 5,000 (elfu tano) vyenye Muhtasari wa MIRADI itakayotekelezwa (2020-2025), vinasambazwa. MIRADI hii inatokana na ILANI mpya ya UCHAGUZI ya CCM ya 2020-2025.
(3) VIPEPERUSHI 5,000 (elfu tano) vya Muhtasari wa WASIFU wa MGOMBE UBUNGE, Prof Sospeter Mwijarubi MUHONGO, vinasambazwa.
(4) VITABU 10,000 (Volume I & II) vyenye TAARIFA za Utekelezaji wa ILANI ya UCHAGUZI ya CCM ya 2015-2020,  usambazaji wake utafikia tamati tarehe 1.10.2020
(5) VIPEPERUSHI 4,200 (elfu nne mia mbili) vya kuvaa shingoni vya WAGOMBEA UDIWANI 21 (@200) wa CCM vinaanza kusambazwa kesho (9.9.2020). Mgombea Ubunge, Prof Muhongo amewatengenezea vipeperushi hivyo.
(6) BENDERA za CCM 500 (400 kutoka Chamani Dodoma & 100 za Mgombea Ubunge) zinagawiwa.
UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM ZA WILAYA YA CCM YA MUSOMA VIJIJINI
Mahali:
Bwai Kwitururu
Kata ya Kiriba
Siku:
Ijumaa, 11.9.2020