PROF. MUHONGO ARUDISHA FOMU ZA MAOMBI YA KUGOMBEA NAFASI YA UBUNGE WA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Ijumaa, 17.7.2020, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Musoma Vijijini, Ndugu Peter Francis Mashenji ALIPOKEA FOMU za Prof Sospeter Muhongo za kuomba kugombea nafasi ya UBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini.
Prof Muhongo alisindikizwa na WASAIDIZI wake 5 {4 wanaotembelea Wanavijiji kila siku wakitumia PIKIPIKI na Dreva 1}. Wasaidizi wengine 3 wako masomoni ambao ni: Webmaster (1) na Wasoma taarifa kwenye On-line Radio (2).