SEKONDARI MPYA ZINADAIWA VYUMBA VIPYA VYA MADARASA KWA AJILI YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA CHA MWAKANI (2021)

Wanafunzi wa Dan Mapigano Memorial Secondary School, wakiwa Darasani.

JIMBO la Musoma Vijijini lina SEKONDARI MPYA 2 (Dan Mapigano Memorial Secondary School, Kata ya Bugoji) & Busambara Secondary School, Kata ya Busambara) zilizofunguliwa Mwaka huu (2020). MIUNDOMBINU ILIYOPO inatosheleza MAHITAJI ya sasa ya KIDATO CHA KWANZA (Form I).
MAOTEO ya Wanafunzi wa FORM I mwakani (2021) ni haya:
(i) Dan Mapigano Memorial Secondary School ya Kata ya Bugoji INATARAJIA KUPOKEA Wanafunzi 250 wa Form I (Jan 2021)
Vyumba Vipya vinavyohitajika ni 5,  vilivyopo ni 2. UJENZI wa Vyumba Vipya 3 umeanza na unapaswa kukamilika kabla ya tarehe 1.10.2020.
Prof Sospeter Muhongo ATACHANGIA MABATI 54 ya Geji 28 (yanayotosha kuezeka darasa moja) kabla ya tarehe 14.7.2020
(ii) Busambara Secondary School  ya Kata ya Busambara INATARAJIA KUPOKEA Wanafunzi 270 wa Form I (Jan 2021)
Vyumba Vipya vinavyohitajika ni 7,  vilivyopo ni 1. UJENZI wa Vyumba Vipya 6 umeanza na unapaswa kukamilika kabla ya tarehe 1.10.2020.
Prof Sospeter Muhongo ATACHANGIA MABATI 54 ya Geji 28 (yanayotosha kuezeka darasa moja) kabla ya tarehe 14.7.2020
SEKONDARI NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI
* Sekondari za Serikali au Kata ni 20.
Ujenzi wa MAABARA kwenye Sekondari zote 20 HAUJAKAMILIKA!
* Sekondari za Binafsi ni 2
* Sekondari zinazojengwa na zimepagwa zifunguliwe mwakani (2021) ni 5: Seka (Kata ya Nyamrandirira), Nyasaungu, Kabegi (zote za Kata ya Ifulifu), Kigera (Kata ya Nyakatende) na Bukwaya (Kata ya Nyegina). Kata nyingine zilizopanga kuanza kujenga Sekondari ya pili ni Etaro, Mugango na Suguti.
UAMUZI WA KUONGEZA HIGH SCHOOLS JIMBONI MWETU
Tunayo MOJA TU, KASOMA High School, Arts subjects (Kata ya Nyamrandirira)
Baraza la Madiwani lilishaamua KUONGEZA High Schools (hasa za MASOMO ya SAYANSI) kwenye Sekondari zifuatazo: (i) Bugwema, (ii) Mtiro, (iii) Mugango na (iv) Mkirira.
KARIBUNI TUCHANGIE ujenzi wa Secondary & High Schools Jimboni mwetu