WADI YA MAMA NA MTOTO YACHANGIWA SARUJI MIFUKO 200

KIKAO CHA WANAWAKE na MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, kilichofanyika kwenye ZAHANATI ya NYEGINA inayojenga WADI ya MAMA na MTOTO.

ZAHANATI YAKIJIJI CHA NYEGINA inapanuliwa kwa kujenga WADI YA MAMA na MTOTO na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo amechangia SARUJI MIFUKO 200.
UJENZI NA UBORESHAJI WA Miundombinu ya HUDUMA za AFYA Jimboni mwetu UNATEKELEZWA kwa USHIRIKIANO mkubwa na mzuri wa WANANCHI na SERIKALI yao.
HUDUMA ZA AFYA JIMBONI
* JUMLA YA ZAHANATI zinazotoa HUDUMA ni: 24 za Serikali na 4 za Binafsi.
* JUMLA YA VITUO VYA AFYA  vinavyotoa HUDUMA ni: 2 (Murangi na Mugango)
UJENZI NA UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU YA AFYA JIMBONI
* HOSPITAL ya Wilaya inajengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, Kijijini Suguti. SERIKALI imechangia Tsh Bilioni 1.5. WANAVIJIJI na MBUNGE wa Jimbo wanachangia ujenzi huu.
* ZAHANATI MPYA 14 zinajengwa kwenye Vijiji 14. Serikali imechangia ujenzi wa Maboma ya Zahanati za Vijiji vya Chirorwe na Maneke.
* ZAHANATI ya Kijiji cha Masinono inapanuliwa iwe KITUO CHA AFYA. Serikali imechangia Tsh Milioni 400. WANAVIJIJI na MBUNGE wa Jimbo watachangia ujenzi huu.
* ZAHANATI YA BUKIMA inajenga WADI YA MAMA na MTOTO na Mbunge wa Jimbo alichangia SARUJI MIFUKO 100 tarehe 13 JUNE 2018. Ujenzi unaenda kwa kasi ndogo.
MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI (8 March 2020) – TUBORESHE HUDUMA ZA AFYA KWA MAMA NA MTOTO, NA KWA FAMILIA NZIMA.