SEKONDARI MPYA JIMBONI KUONGEZA KASI KWENYE UJENZI WA MIUNDOMBINU MIPYA 

VIKAO vya Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo na WANAVIJIJI wa Kata ya Bugoji

DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL ya Kata ya Bugoji yenye Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na iliyofunguliwa Mwaka huu (2020) ITAHITAJI VYUMBA VIPYA 5 VYA MADARASA kwa ajili ya Kidato cha Kwanza cha Mwakani (2021, Maoteo ni Wanafunzi 218). Vipo Vyumba vipya 2 vilivyokamilishwa ujenzi
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL ya Kata ya Busambara yenye Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza na iliyofunguliwa Mwaka huu (2020) ITAHITAJI VYUMBA VIPYA 7 VYA MADARASA kwa ajili ya Kidato cha Kwanza cha Mwakani (2021, Maoteo ni Wanafunzi 270). Lipo Boma la Vyumba 2 vya Madarasa linalojengwa.
UAMUZI WA WANANCHI WA KATA YA BUGOJI
(Dan Mapigano Memorial Secondary School)
* Ujenzi wa Maabara,  Vyoo Matundu 10, Nyumba ya Walimu (two in one) UKAMILIKE kabla ya tarehe 30 JULAI 2020.
* Ujenzi MPYA wa Vyumba 6 vya Madarasa na Nyumba ya pili ya Walimu (two in one) UKAMILIKE kabla ya tarehe 30 AGOSTI 2020.
* FAMILIA MAPIGANO imehudhuria Kikao cha leo (6.3.2020) cha Kijijini Bugoji na  kuhaidi KUJENGA CHUMBA 1 cha Darasa. Baadae watachangia COMPUTERS. Ujumbe wa Familia Mapigano uliongozwa na Ndugu Jarled Lisso.
* Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo aliyeitisha Kikao hicho cha Wananchi wa Kata ya Bugoji. amechangia MBAO za kutengeneza MEZA 6 na VITI 6 (Tsh 2 Million)
UAMUZI WA WANANCHI WA KATA YA BUSAMBARA
(Busambara Secondary School)
* Ifikapo tarehe 30 APRIL 2020 Kijiji cha Maneke kikamilishe ujenzi wa Boma la Vyumba 2 vya Madarasa.
* Ifikapo tarehe 30 APRIL 2020, Vijiji vya Mwiringo na Kwikuba, kila kimoja  kikamilishe ujenzi wa Vyumba vipya 2 vya Madarasa.
* Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo aliyeitisha Kikao cha leo (6.3.2020) Kijijini Kwikuba amechangia RANGI za KUPAKA Ofisi ya Walimu, na Vyoo vya Wanafunzi na Walimu.
WANAVIJIJI WA KATA ZA BUSAMBARA NA BUGOJI WANAWAOMBA WAZALIWA WA KATA HIZO WAUNGANE NAO KWENYE UJENZI WA SEKONDARI MPYA HIZO