WASAGA FC YAENDELEZA MATUMAINI YA KUWA MABINGWA WA MKOA

WASAGA FC ya Kijijini Kasoma

Jumatano, 15.1.2020
Jimbo la Musoma Vijijini
Timu ya WASAGA FC inayoshiriki Ligi  Daraja la Tatu Mkoani Mara imeendelea kufanya vizuri katika mashindano ya Ligi hiyo.
WASAGA FC ni Timu ya Kijiji cha Kasoma, Kata ya Nyamrandirira. Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo ametoa MCHANGO MKUBWA (usajiri/posho, jezi na viatu) kuiwezesha Timu hii kushiriki Ligi hiyo.
Katika Mchezo wa kwanza wa tarehe 6 Januari 2020, WASAGA FC ilishinda bao 1 – 0 dhidi ya Timu ya JK FC ya Manispaa ya Musoma na kutinga hatua ya nusu fainali.
Mchezo wa Nusu Fainali uliofanyika tarehe 13.01.2020 kati ya Timu ya WASAGA FC na TAGOTA ya Tarime, Timu ya WASAGA FC iliibuka na ushindi wa mabao 2 – 0. Ushindi huo ulitosha kuipeleka WASAGA FC fainali ambapo itacheza na NYAMONGO SC ya Tarime tarehe 16 Januari 2020 kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume Mjini Musoma