MBUNGE WA JIMBO AIWEZESHA TIMU YA KIJIJI CHA KASOMA KUSHIRIKI LIGI DARAJA LA 3

MSAIDIZI wa Mbunge, Ndugu Fedson Masawa (mwenye track suit) akikabidhi JEZI na VIATU kwa VIONGOZI na WACHEZAJI wa Wasaga FC., Kijijini Kasoma, Makao Makuu ya Wasaga FC.

MICHEZO na UTAMADUNI ni moja ya VIPAUMBELE vya Jimbo la Musoma Vijijini lenye Vitongoji 374, Vijiji 68 na Kata 21.
TIMU YA WASAGA FC ya Kijiji cha Kasoma, Kata ya Nyamrandirira inashiriki LIGI YA DARAJA LA 3 ya Mkoa wa Mara.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo AMEIWEZESHA WASAGA FC kushiriki LIGI hiyo kwa kuchangia:
* USAJILI wa Wachezaji
* Jezi Mpya
* Viatu vya kuchezea Mpira wa Miguu
VIFAA hivyo vimekabidhiwa kwa TIMU hiyo tarehe 12.1.2020
Vilevile, Mbunge huyo wa Jimbo la Musoma Vijijini ni mmoja wa Wafadhili wa BIASHARA UNITED ya Mkoa wa Mara inayoshiriki LIGI KUU ya Taifa.