MICHEZO JIMBONI – UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM YA 2015-2020

Mashindano ya kupiga Kasia yaliyofanyika Kijijini Bukima, tarehe 30.12.2019.

Mashindano ya Kupiga Kasia (AINA MOJAWAPO YA MCHEZO) yaliyofanyika jana (30.12.2019) Kijijini Bukima ni sehemu ya UTEKELEZAJI wa ILANI ya CCM ya 2015-2020.
Mbunge wa Jimbo la la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo AMEAMUA KIVITENDO KUFUFUA Utamaduni na Michezo ya Jimboni mwao iliyokuwa INAFIFIA na kuanza KUTOWEKA.
Kila Mwaka, Mbunge huyo anatayarisha na kufadhili MASHINDANO ya KWAYA (nyimbo) na NGOMA ZA ASILI.
Vilevile, Mbunge huyo ni mmoja wa WAFADHILI wa Timu ya Mpira ya Mkoa wa Mara, BIASHARA UNITED inayoshiriki Ligi Kuu ya Taifa. Ameombwa na kukubali kuna mmoja wa Wafadhili wa WASAGA FC ya Kata ya Nyamrandirira itakayoshiriki Ligi ya Daraja III. Mbunge huyo alishagawa Vifaa vya Michezo Vijijini na Mashuleni.
MASHINDANO YA KUPIGA KASIA 2019 (The Annual Boat Race) – Washindi na Zawadi
Mbunge wa Jimbo ametoa ZAWADI hizi:
MSHINDI 1
Kata ya Murangi
Tsh Milioni 1 & Kikombe
MSHINDI 2
Kata ya Musanja
Tsh 700,000 & Kikombe
MSHINDI 3
Kata ya Suguti
Tsh 400,000 & Kikombe
Mshindi wa Nne
Kata ya Bukima
Mshindi wa Tano
Kata ya Rusoli
ZAWADI ndogo ndogo nazo zilitolewa.
Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini wameomba Mbunge wa Jimbo lao AENDELEE kutayarisha MASHINDANO ya kupiga KASIA na ikiwezekana yafanyike mara mbili kwa Mwaka.