MBUNGE WA JIMBO ATUMIA SIKU ZA KAMPENI KUHAMASISHA UKAMILISHWAJI WA UJENZI WA SEKONDARI MPYA

Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo akieleza MAFANIKIO kutoka kwenye UTEKELEZAJI wa Ilani ya CCM kwa muda wa MIAKA 3 na NUSU (Jan 2016-Juni 2019). Alitumia FURSA hiyo kuhimiza ukamilishwaji wa ujenzi wa Sekondari MPYA za Kata za Bugoji na Busambara.

WANAVIJIJI wa Kata za BUGOJI na BUSAMBARA wamehimizwa kukamilisha ujenzi wa Sekondari zao ili zianze kuchukua Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza (Form I) mwakani, Januari 2020.
Hadi kufikia leo (20.11.2019). Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo tayari ametembelea Kata 20 kati ya Kata 21 za Jimbo hilo AKIELEZA MAFANIKIO yaliyokwishapatikana kutoka kwenye UTEKELEZAJI wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2015-2020). Amefanya VIKAO vya ndani (na nje kwa baadhi ya Kata) na WAGOMBEA wa CCM wa ngazi zote kwenye Kata zote hizo 20 na moja iliyobaki ataikamilisha baada ya kutoka kazini kwenye Jimbo la Butiama.
DAN MAPIGANO MEMORIAL SECONDARY SCHOOL (Kata ya Bugoji)
VILIVYOKAMILIKA:
*Vyumba 5 vya Madarasa
*Madawati 40 kila Darasa
*Ofisi 2 za Walimu
*Viti na Meza za Ofisi za Walimu
UJENZI UTAKAOKAMILIKA KABLA YA TAREHE 15 DEC 2019:
*Matundu 10 ya Vyoo vya Wasichana
*Matundu 10 ya Vyoo vya Wavulana
*Matundu 2 ya Vyoo vya Walimu
*MAABARA 3 (Physics, Chemistry & Biology)
*NYUMBA ya Mwalimu Mkuu
NB: Mfuko wa Jimbo umechangia ujenzi huo (Kata  ya Bugoji) SARUJI MIFUKO 290 na NONDO 100.
BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL (Kata ya Busambara)
VILIVYOKAMILIKA:
*Vyumba 4 vya Madarasa
*Madawati 40 kila Darasa
UJENZI UTAKAOKAMILIKA KABLA YA TAREHE 15 DEC 2019
*Ofisi 3 za Walimu (Viti na Meza zake)
*Matundu 8 ya Vyoo vya Wasichana
*Matundu 6 ya Vyoo vya Wavulana
*Matundu 2 ya Vyoo vya Walimu
*MAABARA 3 (Physics, Chemistry & Biology)
*NYUMBA ya Mwalimu Mkuu
NB: Mfuko wa Jimbo umechangia ujenzi huo (Kata ya Busambara) SARUJI MIFUKO 290 na NONDO 100.