VIKUNDI VYA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI VYACHANGAMKIA MIKOPO KUTOKA JAMII IMPACT LIMITED

UZINDUZI wa OFISI ya JAMII IMPACT LIMITED kwenye eneo la Kanisa la Mennonite (KMT), Nyabange.

Taasisi ya JAMII IMPACT Limited inatoa huduma ya MIKOPO kwa VIKUNDI vinavyojishughulisha na MIRADI ya KI-UCHUMI vikiwemo VICOBA vilivyo na utaratibu wa kununua hisa na kukopeshana.
VIKUNDI kadhaa vya Jimbo la Musoma Vijijijini kutoka Kata za Nyambono, Suguti, Kiriba, Ifulifu na Nyakatende VIMEJITOKEZA na kutuma maombi yao.
Kikundi cha TUMAINI VICOBA GROUP cha Kata ya Kiriba KIMETIMIZA MASHARTI ya Ombi la MKOPO wao. Kikundi hiki chenye WANACHAMA 30 kinajihusisha na shughuli za kilimo, ufugaji, uvuvi na biashara. Fedha za MKOPO zitatolewa kwa ajili ya shughuli za ki-uchumi za Kikundi hiki.
JAMII IMPACT LIMITED inakaribisha  VIKUNDI vingine kupeleka MAOMBI yao ya MIKOPO kwenye OFISI zao  zilizopo NYABANGE KMT Mission, Musoma.
Kwa MAELEZO zaidi, Wasiliana na:
Ndugu William Mdemu
Namba: 0658218673 / 0758208673
Afisa Mikopo (Jamii Impact Limited)