MBUNGE WA JIMBO AENDELEA KUCHANGIA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

MAKABIDHIANO ya PRINTER MPYA Ofisini kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Musoma Vijijini. Msaidizi wa Mbunge, Ndugu Fedson Masawa (kushoto) alimkabidhi Katibu wa CCM Wilaya, Ndugu Stephen Koyo (wa pili kushoto) PRINTER MPYA iliyonunuliwa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini.

Leo, Jumatano, tarehe 23.10.2019, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo, AMENUNUA PRINTER MPYA kwa ajili ya matumizi kwenye OFISI ya CCM ya Wilaya ya MUSOMA VIJIJINI. Hapo awali aliinunulia Ofisi hii COMPUTER MPYA.
Vifaa hivyo ni muhimu sana kwa wakati huu wa matayarisho ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 24.11.2019.
Vilevile, Mbunge huyo AMECHANGIA JUMLA ya LITA 400 (mia nne) za Dizeli kwa ajili ya ZIARA za shughuli za UCHAGUZI za Kamati ya Siasa na Sekretariati ya CCM ya Wilaya ya Musoma Vijijini.
CCM Wilaya ya BUTIAMA imepokea JUMLA ya LITA 300 za Dizeli kutoka kwa Prof Sospeter Muhongo ikiwa ni MCHANGO wake kwa ajili ya matayarisho ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wilayani BUTIAMA.
CCM Mkoa imechangiwa LITA 200 za Diseli na Prof Sospeter Muhongo. MAFUTA haya ni kwa ajili ya Ziara za Viongozi wa Mkoa kwenye shughuli za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.