RATIBA YA KUMBUKIZI YA BABA WA TAIFA 

Mgeni Rasmi, Mhe Jaji Joseph Sinde Warioba akitoa zawadi mbalimbali kwa Washindi wa Ngojera na Hotuba za Baba wa Taifa

Kila siku, kuanzia tarehe 08 Okt hadi 14 Okt kuna MASHINDANO ya Michezo mbalimbali ikiwemo riadha, mpira wa pete na miguu, bao na baiskeli. Kwaya na Ngoma za Asili nazo zipo.
Jumamosi, 12.10.2019, Makumbusho ya Mwalimu Nyerere Butiama chini ya Uongozi wa Mkurugenzi wake, Ndugu Emmanuel Kiondo walitayarisha MASHINDANO ya Shule za Msingi na Sekondari ya NGONJERA na HOTUBA ZA BABA WA TAIFA yakipima viwango vya vipaji vya Wanafunzi hao kwenye KUMBUKUMBUKU ya kazi za Baba wa Taifa. Vilevile kwenye kuelezea WASIFU wake.
Mgeni Rasmi wa Mwaka huu (2019) ni Jaji Joseph Sinde Warioba. Wageni wengine ni Ndugu Philip Mangula na Ndugu Stephen Masato Wasira.
 MATUKIO mbalimbali yamefanyika Mwitongo, eneo la Makumbusho ya Mwalimu Nyerere.