KARIBUNI TUKAMILISHE UJENZI WA BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL

ujenzi wa Vyoo vya Wanafunzi. Majengo ya rangi nyeupe ni Vyumba vya Madarasa, na kulia ni Jengo la Utawala.

Leo, Jumatano, 09.10.2019, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo AMEFANYA UKAGUZI MWINGINE ndani ya mwezi mmoja, wa ujenzi wa Busambara Secondary School ya Kata ya Busambara.
MAJENGO YANAYOPASWA KUKAMILISHWA
* Vyoo vya Wanafunzi na Walimu
* Maabara za Physics, Chemistry and Biology
* Nyumba ya kuishi Mwalimu Mkuu
SHUKRANI:
Tokea jana, Jumanne, 08.10.2019, naona WAZALIWA  wa Vijiji vya Maneke, Kwikuba na Mwiringo, yaani Kata ya Busambara, WANAHIMIZANA KUTOA MICHANGO ili Busambara Secondary School ifunguliwe na ianze kutoa Elimu ya Sekondari Januari 2020.
KARIBU UCHANGIE UJENZI WA BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL