CHAMA CHA MAPINDUZI KATA YA RUSOLI YAMTUNUKU MHE. MBUNGE WA JIMBO HATI YA HESHIMA.

Msaidizi wa Mbunge akionesha hati ya HESHIMA aliyokabidhiwa Mh. Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo

HATI hii ya HESHIMA  ni kielelezo cha WANA-RUSOLI kutambua MCHANGO MKUBWA wa MAENDELEO anaoutoa Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo kwenye Kata ya Rusoli.
HATI imekabidhiwa na M/kiti wa CCM Kata ya Rusoli Ndugu Sabato Mkome, kwa Msaidizi wa Mbunge Hamisa Gamba, leo tarehe 6/9/2019, kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo.
Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo
ameishukuru sana CCM  Kata ya Rusoli, kwa kutambua MCHANGO WAKE MKUBWA kwenye Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2015-2020) kwenye Kata hiyo na ndani ya Kata zote za Jimbo la Musoma Vijijini.