WANAKAZI WA KIJIJI CHA KAKISHERI WACHOSHWA KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA HUDUMA ZA AFYA

Kikao cha Tarehe 01.06.2019 cha WANANCHI, Mbunge wa Jimbo, Viongozi wa CCM Wilaya, kwenye eneo la ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kakisheri, Kata ya Nyakatende.

Jumamosi 01.06.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Wakazi wa Kijiji cha Kakisheri, Kata ya Nyakatende WANALAZIMIKA kutembea umbali wa kilomita 4 kwenda kwenye Zahanati ya Kijiji jirani cha Kiemba kupata MATIBABU wanapoyahitaji. HUDUMA za Afya nyingine zinapatikana Musoma Mjini, umbali wa kilomita 15 kutoka Kijijini Kakisheri.
Kutokana na kero hiyo SUGU ya upatinakanaji wa HUDUMA za AFYA, Wakazi wa Kijiji cha Kakisheri WAMEAMUA kujenga Zahanati Kijijini mwao.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, Ndugu Msafiri Kolesi ameeleza kwamba WANANCHI wamekubali KUJITOLEA kutumia NGUVUKAZI zao kujenga Zahanati yao. Wanasomba mawe, kokoto, mchanga na maji. Vilevile kila KAYA inachangia Tshs 23,000 kwa ujenzi huu unaosimamiwa na Viongozi wa Kijiji na Kaimu Mtendaji wa Kijiji, Ndugu Antony Ndege.
Diwani wa Kata hiyo, Mhe Rufumbo Mugini Rufumbo amesema ujenzi wa Zahanati hiyo UTAENDA KWA KASI kubwa zaidi baada ya Wana-Kakisheri kukamilisha UJENZI wao wa Vyumba 2 vya Madarasa kwenye Sekondari yao ya Kata (Nyakatende Secondary School). Ujenzi huu wa Vyumba vya Madarasa ulikuwa muhimu ili kuhakikisha Wanafunzi wa Kijiji cha Kakisheri WALIOFAULU na KUCHAGULIWA kuanza Form I kwenye Sekondari ya Nyakatende WANAANZA MASOMO yao bila kuchelewa.
MBUNGE WA JIMBO ATIMIZA AHADI YAKE LEO
Baada ya kukagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kakisheri, Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo amechangia leo SARUJI MIFUKO 50 kama alivyoahidi.
Mbunge huyo alitembelea eneo la ujenzi akiwa amefuatana na Katibu ya CCM Wilaya, Ndugu Stephen Koyo na Viongozi wengine wa Chama (CCM)