UJENZI WA SHULE SHIKIZI YA KIJIJI CHA BUANGA WAFIKIA HATUA NZURI

Ujenzi wa Miundombinu ya Shule Shikizi ya Kijiji cha Buanga, Kata ya Rusoli

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
Ijumaa 31.05.2019
Watoto wa Kijiji cha Buanga, Kata ya Rusoli, wanalazimika kutembea umbali usiopungua kilomita 3-5 kwenda masomoni kwenye Shule ya Msingi Bwenda iliyoko Kijiji jirani – utoro, mimba na matokeo hafifu ya mitihani ni baadhi ya athari zinazotokana na mazingira hayo ya Elimu Kijijini Bwanga  – hayo yamesemwa na Mwl James William ambae ni Mlezi wa Shule Shikizi inayojengwa na ndie Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Bwenda.
Kwa hiyo, Wananchi wa Kijiji cha Buanga WAMEAMUA kujenga Shule SHIKIZI Kijijini mwao wakikusudia hapo mbeleni kuipanua na kuwa Shule kamili ya Msingi inayojitegemea.
Ujenzi wa Shule Shikizi ya Buanga umefikia hatua nzuri ambapo Boma moja la Vyumba Viwili (2) vya Madarasa na Ofisi moja (1) ya Walimu liko kwenye hatua ya ukamilishwaji.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Buanga, Ndugu Kejire Eyembe ameelezea MAFANIKIO ya ujenzi huo kuwa, mbali na MICHANGO ya Wadau mbalimbali na Diwani wao, WANANCHI wa Kijiji cha Buanga wanachangia Nguvukazi kwa kusomba Mawe, Mchanga na Maji. Vilevile kila KAYA inachangia fedha taslimu, Tsh 10,000/= (elfu kumi).
Mwenyekiti huyo ameendelea na kusema kwamba kazi iliyoko mbele yao ni: kupaua na kukamilisha ujenzi wa BOMA hilo na kujenga matundu 10 ya CHOO ya Wanafunzi, na matundu 2 ya CHOO ya Walimu. Vilevile kuna ujenzi wa nyumba ya Mwalimu.
Diwani wa Kata ya Rusoli Mhe Boaz M. Nyeula amewashukuru WADAU mbalimbali wanaochangia ujenzi wa Shule ya Buanga akiwemo Mbunge wa Jimbo lao Prof Muhongo kwa MCHANGO wake binafsi wa SARUJI MIFUKO 50 na MCHANGO na Mfuko wa Jimbo SARUJI MIFUKO 50.
WAZALIWA na WADAU wa Maendeleo waliokwisha CHANGIA ujenzi huu ni:-
1. Jackison Songora
2. Nyabwira Mugonya
3. Jeremia Mugonya
4. Lawrance Wegoro
5. Samson Mbogora
6. Hamis Mgaya
7. Nyang’ura Masatu
8. Shida Samamba
9. Masau Mashauri
10. Emanuel Kusaga
Diwani wa Kata Mhe Nyeula na Mwenyekiti wa Kijiji Ndugu Eyembe wanaomba WAZALIWA wa Kata ya Rusoli na WADAU wengine wa Maendeleo KUJITOKEZA na KUCHANGIA ukamilishaji wa Shule Shikizi ya Kijiji cha Buanga.
Viongozi hao wanaendelea KUMSHUKURU sana Mbunge wa Jimbo, Prof Muhongo kwa kubaini MICHANGO yake mingine  katika Sekta ya Elimu kwenye S/M Bwenda A&B ambapo hadi sasa amechangia  SARUJI MIFUKO 120, MADAWATI 162 na VITABU vingi.