UJENZI WA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MKIRIRA WAENDELEA VIZURI

FUNDI akiendelea na ujenzi wa Boma la Zahanati ya Kijiji cha Mkirira

Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Jumamosi 25.05. 2019
UJENZI wa Zahanati ya Kijiji cha Mkirira, Kata ya Nyegina unaendelea vizuri baada ya kusuasua kwa miezi michache ya nyuma. Boma linapandishwa vizuri kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini. Maendeleo hayo mazuri yanazidi kuwapa MATUMAINI makubwa Wananchi wa Kijiji cha Mkirira kwani LENGO LAO KUU la upatikanaji wa Huduma ya Afya Kijijini mwao litafikiwa hivi karibuni.
Diwani wa Kata ya Nyegina, Mhe Majira Mchele amemueleza Msaidizi wa Mbunge, Ndugu Fedson Masawa kuwa mafanikio ya ujenzi wa Zahanati hiyo yanatokana na UMOJA na MSHIKAMANO kati ya Wazaliwa wa Kijiji cha Mkirira waishio nje ya Kijiji hicho na  Wazazi, Ndugu na Jamaa zao walioko hapo Kijijini (nyumbani kwao).
Wazaliwa wa Kijiji cha Mkirira walioanza kuchangia Ujenzi wa Zahanati hiyo ni:
(1) Joackim Masumbuko Nyarigo
(2) Dr med Happy Lisso
(3) Beatus John Malima
(4) Boko Dioniz Majinge
(5) Hamis Mbagati Nyarigo
(6) Joseph Nyerere
(7) Rose Nyarigo
(8) Juma Madibi
(9) Nyabise Mbagati Nyarigo
(10) Hasira Masige
(11) Zitta Dioniz Majinge
(12) Fikiri Jumanne Wantai
(13) Gwabhala Msira
Wadau wengine wa Maendeleo nao WANACHANGIA ujenzi huu. Mhe Diwani Majira amewashukuru sana, ambao ni:
(14) Wananchi wa Kijiji cha Mkirira na Diwani (yeye) kwa kusomba Maji, Mchanga, Mawe na kuchanga Fedha za kumlipa Fundi.
(15) Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo amechangia SARUJI MIFUKO 200
(16) Mbunge Viti Maalum, Mhe Amina Makiragi amechangia SARUJI MIFUKO 180
(17) Kampuni ya Nyanza Road imechangia SARUJI MIFUKO 50 na TRIPU 7 za KOKOTO.
Kaimu Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mkirira, Ndugu Pascal Eliga ambae ndiye Msimamizi Mkuu wa ujenzi wa Zahanati hiyo  amesema bado wana ukosefu wa NONDO 100 ili waweze kuharakisha ukamilikaji wa BOMA hilo mapema kabla tarehe 30 June 2019.
UONGOZI wa Serikali ya Kijiji cha Mkirira, kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji hicho wanathamini sana MICHANGO ya NDUGU ZAO waishio nje ya Mkoa wa Mara na Wadau wengine wote wa Maendeleo kwa kuchangia ujenzi huo. WANAWAOMBA wazidi KUJITOLEA kutoa MICHANGO YAO ili kukamilisha ujenzi wa Zahanati hiyo mapema iwezekanavyo, kabla ya Januari 2020.