BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL

Baadhi ya MAJENGO (yanayokamilishwa) ya Busambara Secondary School

Jumanne, 28.05.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
LENGO:
*August 2019 Secondary IANDIKISHWE na kutambuliwa na Serikali.
*January 2020  Secondary IANZE kuchukua Wanafunzi wa FORM I wengi wao wakitoka Vijiji vya Maneke, Kwikuba na Mwiringo (Kata ya Busambara)
WACHANGIAJI WA UJENZI WA BUSAMBARA SECONDARY SCHOOL
(1) WANAVIJIJI:
(a) kutoka VIJIJI  vyote 3 wanasomba mawe, kokoto, mchanga na maji. Wanatengeneza tofali na kusaidia MAFUNDI kwenye ujenzi.
(b) Kila KAYA au kila NGUVUKAZI ndani ya Kata ya  Busambara IMECHANGIA na inaendelea KUCHANGIA Fedha taslimu kati ya Tsh 3,000 na 10,000 kwa ajili ya ujenzi huu.
(c) Harambee 2 zilishapigwa kwenye eneo la ujenzi wa Sekondari.
(2) VIONGOZI wa CCM wa Kata na Vijiji na DIWANI wa Kata (CHADEMA) wanachangia ujenzi huu.
(3) VIONGOZI wa Serikali wakiwemo Watendaji wa Vijiji na Kata wanachangia ujenzi huu.
(4) HALMASHAURI YETU inachangia ujenzi huu.
*DED wetu Ndugu John Kayombo anasimamia kwa umakini mkubwa ujenzi huu.
(5) MFUKO wa JIMBO: umechangia MABATI 75
(6) MBUNGE wa JIMBO Prof Sospeter Muhongo anachangia ujenzi huu na ameishatoa: SARUJI MIFUKO 150 na MABATI BANDO 8 (Mabati 96)
(7) NMB (Benki): itachangia MEZA 80 na VITI 80
(8) WAZALIWA wa KATA ya BUSAMBARA: Ndugu zetu waliozaliwa au WAZAZI/UKOO wao wana/una chimbuko la Kata ya Busambara WAMEAMUA KUCHANGIA ujenzi huu na  AHADI ZINATIMIZWA kama ifuatavyo:
(8a) Ndugu Joseph Chikongoye amechangia Tsh 500,000
(8b) ACP Nyakulinga amechangia Tsh 1,000,000
(8c) Wakili/Mchumi Saidi Chiguma amechangia Tsh 500,000.
*DC wetu Dr Vicent Naano Anney ANASIMAMIA VIZURI sana Michango yote inayotolewa.
Hadi sasa MAJENGO yaliyoezekwa na yanayokamilishwa ujenzi ni:
(i) Vyumba vya Madarasa 4 na Ofisi 2 za Walimu
(ii) Jengo la Utawala
TUNAOMBWA TUCHANGIE UJENZI wa SEKONDARI YETU IKAMILIKE kabla ya tarehe 01.08. 2019.