WAZALIWA WA KATA YA NYAMBONO WATEKELEZA AHADI ZAO KWA VITENDO: JENGO LA OPD LA KITUO CHA AFYA NYAMBONO LAKARIBIA KUEZEKWA

Mafundi wakiwa kwenye Ukamilishaji wa Renta ya Jengo la OPD la Kituo cha Afya Nyambono

Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
WAZALIWA wa Kata ya Nyambono yenye Vijiji 2 (Nyambono na Saragana) wameendelea kushirikiana na Wazazi, Ndugu na  Jamaa zao huko nyumbani kwako KUJENGA KITUO CHA AFYA cha Kata ya NYAMBONO kwa njia ya KUJITOLEA.
WANANCHI wa Kijiji cha Nyambono wamekubali KUJITOLEA kusomba maji, mawe, mchanga na kokoto na michango ya fedha taslimu ambayo kila KAYA inachangia Tsh. 11,000/= (elfu kumi na moja).
Sambamba na Jitihada hizo za WANANCHI, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo ameunga mkono Jitihada zao kwa kuchangia SARUJI MIFUKO 100 na NONDO 18.
WAZALIWA au wenye chimbuko la Kijiji cha Nyambono ambao kwa sasa wanaishi nje ya Kijiji hicho ndio walioanzisha MRADI huu wa ujenzi. WAMEANZA KUCHANGIA tokea hatua za awali kabisa (foundation) za UJENZI wa Kituo hiki cha Afya.
Hivi karibuni wamechanga Tsh  5,954,000/= kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi vya kukamilisha renta ya Jengo la OPD.
Aidha Uongozi wa Kijiji na Kata ya Nyambono, ukiongozwa na Diwani wa Kata ya Nyambono Mhe Mkoyongi Masatu Nyanjaba umetoa shukrani za pekee kwa WADAU WOTE wanaochangia ujenzi wa Kituo cha Afya Nyambono ambao ni: Wananchi, Wazaliwa wa Nyambono na Mbunge wa Jimbo.
Orodha ya WADAU WACHANGIAJI kwa upande wa WAZALIWA wa Nyambono ni:
1. Mkama Manyama
2. Nice Kuleba
3. Majura Songo
4. Eliud Kwabira
5. Shida Mlegi
6. Beredy Maregesi
7. Maganira Daudi
8. Malenya Sambu
9. David Alal
10. Bunyata Mkama
11. Adonias Mkama
12. Japhet Maganira
13. Mch. Yeremia Magomba
14. Ominde John
15. Albinus Manumbu
16. Benedict Mkama
17. Dickson Mufungo
18. Ching’oro Ebanda, na wengine wote wanaoendelea kutoa ushirikiano na michango yao kwenye ujenzi wa Kituo cha Afya cha Nyambono.
“Kazi bado ni kubwa, MCHANGO wako ni muhimu.” Karibu Tujenge Kituo cha Afya Nyambono.