WANAFUNZI 133 WA FORM I WA SHULE YA SEKONDARI BUKIMA WALIOSUBIRI UPATIKANAJI WA VYUMBA VYA MADARASA  WAANZA MASOMO

Wanafunzi wa Form I wa Bukima Secondary School wakiwa masomoni Shuleni hapo

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
Jumamosi, 28.04.2019
Wanafunzi 133 wa Shule ya Sekondari Bukima waliokuwa wamekosa nafasi ya kujiunga na Kidato cha Kwanza (Form I) kutokana na uhaba wa Vyumba vya Madarasa tayari WAMEANZA Masomo yao ya Form I baada ya kukamilika kwa Vyumba 2 vya Madarasa Shuleni hapo.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Elbert Deogratias amesema, “Kukamilika kwa Vyumba viwili vya Madarasa Shuleni hapa kumewezesha Wanafunzi waliokuwa nyumbani sasa wameanza Masomo yao ya Form I.”
Mwalimu Mkuu huyo aliendelea kueleza kwamba hadi sasa wanavyo Vyumba vya Madarasa vitatu (3) kwa Form I na kila Darasa wanakaa Wanafunzi 62.
Diwani wa Kata ya Bukima, Mhe January Simula anamshukuru sana Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo kwa kutoa KIPAUMBELE cha kuboresha Miundombinu ya  Shule za Msingi na  Sekondari Jimboni mwao, na kubwa zaidi ni lile la Mbunge wa Jimbo kushirikiana na Wananchi na Wadau wa Maendeleo  kukamilisha Vyumba vya Madarasa ili kila Mwanafunzi aliyefaulu na kuchaguliwa kuendelea na Masomo ya Sekondari (Form I) anaenda Shuleni si kubaki nyumbani.
Diwani Simula amebainisha kwamba kwa Ukamilishaji wa ujenzi wa Vyumba vya Madarasa kwenye Sekondari ya Bukima, Mbunge wao amewachangia SARUJI MIFUKO 50.
Fedha za MFUKO wa Jimbo zimewapatia SARUJI MIFUKO 100 na MABATI 58
Vijiji  3 vya Kata ya Bukima, yaani Kijiji cha Kastam, Butata na Bukima vimeshirikiana vizuri sana kuhakikisha ujenzi huo unakamilika mapema na Wanafunzi wanaenda kuanza Masomo ya Sekondari (Form I) badala ya kukaa nyumbani kwa ukosefu wa Vyumba vya Madarasa.
Mafanikio haya yamechangiwa na DC, Dr Vicent Anney na DED, Ndugu John Kayombo – Diwani, kwa niaba ya Kata ya Bukima, anatoa shukrani nyingi kwa Viongozi hawa wawili ambao nao walihakikisha Wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kwenda Sekondari wanaenda masomoni badala ya kukaa nyumbani kwa ukosefu wa Vyumba vya Madarasa.
Diwani Mhe January Simula ameendelea kumshukuruku Mbunge wao kwa MICHANGO MIKUBWA ya MBEGU (Alizeti, Mihogo, Mtama), SARUJI, MABATI, MADAWATI na VITABU aliyotoa   kwenye Kata hiyo ikiwemo ya kuchangia ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Butata na Wadi la Mama na Mtoto kwenye Zahanati ya Bukima.
UONGOZI na WANANCHI wa Kata ya Bukima bado wanakaribisha MICHANGO ya Uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu na Afya kwenye Kata yao.