MAKTABA YAZINDULIWA KISIWANI RUKUBA – ZAWADI YA PASAKA KWA WAKAZI WA KISIWA HICHO 

Safari za BOTI za kwenda na kurudi kutoka Kisiwani Rukuba

Shule ya Msingi ya Rukuba iliyoko Kisiwani Rukuba, Kata ya Etaro imesherehekea UZINDUZI wa MAKTABA ya Shule yao. Mbunge wa Jimbo Prof Sospeter Muhongo ndiye aliyezindua Maktaba hiyo.
Maktaba hiyo ina VITABU mchanganyiko vikiwemo vya ngazi zote za Shule na vingine vya kuongeza MAARIFA (knowledge) ya aina mbalimbali. Hii Maktaba itatumiwa na Wanafunzi, Walimu, Wananchi na hata Wageni wanaotembelea Kisiwa cha Rukuba. Kwa hiyo ni Maktaba ya Jamii (Community Library). Mbunge Prof Muhongo AMEHAIDI kuendelea kuipatia MAKTABA hiyo VITABU zaidi.
S/M Rukuba ni MFANO WA KUIGWA – ina Vyumba 11 vya Madarasa (hawapo Wanafunzi wanaosomea chini ya MITI). Walimu wanayo Ofisi yao. Mwalimu Mkuu anayo Ofisi yake peke yake. Walimu wote wanazo nyumba nzuri za kuishi, n.k. na sasa wamepata  MAKTABA!
Kisiwa cha Rukuba kinafungia UMEME wa SOLA.
VIONGOZI wa CHAMA na SERIKALI wa ngazi mbalimbali wamehudhuria uzinduzi huu, akiwemo Katibu wa Chama (CCM) wa Wilaya Ndugu Stephen Koyo.
WANANCHI wakiwemo WANAFUNZI wameshiriki kwenye Chakula cha pamoja cha PASAKA (Easter Lunch).