UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA YA  MRADI WA SERIKALI WA EP4R WATEKELEZWA KIJIJINI CHIRORWE

Mafundi wakiwa kazini wakitekeleza Mradi wa EP4R kwenye Shule ya Msingi Chirorwe.

Alhamisi, 02.05.2019
Jimbo la Musoma Vijijini
Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
Wananchi wa Kijiji cha Chirorwe kilichoko Kata ya Suguti hivi karibuni wameanza UTEKELEZAJI wa MRADI wa EP4R {Education Programme for Results} wa Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa ya Shule ya Msingi Chirorwe.
Ujenzi huo wa Vyumba Viwili (2) na Ofisi 1, pamoja na Matundu Saba (7)  ya Vyoo unaoendelea Shuleni Chirorwe umewapatia Tsh Milioni 46.6 kutoka Serikalini.
Diwani wa Kata ya Suguti, Mhe Denis Ekwabi ANAISHUKURU sana SERIKALI kwa kuchangia ujenzi huu  na ameongeza kwa kusema MCHANGO wa Wananchi kwenye Mradi huu ni KUJITOLEA kufanya kazi ikiwa ni njia ya KUSHIRIKIANA na SERIKALI kuboresha MIUNDOMBINU ya ELIMU Shuleni hapo.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Chirorwe, Ndugu Msai Maingu amesema kuwa WANANCHI wameishachangia
Mawe tripu 22, Mchanga tripu 28,  Kokoto tripu 4 na wanasomba Maji ya ujenzi.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Chirorwe Ndugu Martha H. John ameeleza kuwa ujenzi huo utakamilika na MAJENGO kukabidhiwa mwanzoni mwa Mwezi ujao, Juni 2019.
Aidha, Uongozi wa Kijiji cha Chirorwe na Kata ya Suguti kwa ujumla wanatoa shukrani za pekee kwa Mbunge wao Prof Muhongo kwa Jitihada za Maendeleo anazozifanya Jimboni.
MICHANGO ambayo Mbunge wao alishatoa Kijijini Chirorwe, na S/M Chirorwe inajumuisha:
(i) Saruji Mifuko 60 – ambayo iliyotumika kwenye ujenzi wa awali wa Boma la Vyumba  2 vya Madarasa na Ofisi 1.
(ii) Box 10 za Vitabu, zaidi ya Vitabu 1,000
(iii) Madawati 60
(iv) Kijiji cha Chirorwe kilishapokea Mbegu za Alizeti, Mihogo na Mtama kutoka kwa Mbunge wao Prof Muhongo.
Wazaliwa wa Kijiji cha Chirorwe na WADAU wengine wa Maendeleo WANAOMBWA kuchangia UBORESHAJI wa Miundombinu ya ELIMU na AFYA ya Kijiji cha Chirorwe.
“Kutoa ni Moyo, karibuni Tuchangie Maendeleo ya Kijiji cha Chirorwe”.