WANANCHI WA KISIWA CHA RUKUBA WAANZA MAANDALIZI YA UJENZI WA WODI YA MAMA NA WATOTO

Wanachi wa Kisiwa Rukuba wakiendelea na Usombaji wa Mchanga wa kujengea Wodi ya Mama na Watoto.

Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Wakazi wa Kisiwa cha Rukuba kilichopo Kata ya Etaro wameanza maandalizi ya ujenzi wa Wodi ya MAMA na WATOTO kwenye Zahanati ya Kisiwa/ Kijiji chao. Wameanza kusomba MCHANGA na MAWE ya ujenzi huo.
Muuguzi wa Zahanati ya Rukuba Ndugu Jovin Mafuru alimweleza Msaidizi wa Mbunge (Ndugu Fedson Masawa) kwamba UAMUZI wa kujenga Wodi ya MAMA na WATOTO umefanywa na Wananchi wenyewe ikiwa ni muendelezo wa UBORESHAJI wa HUDUMA za AFYA katika Kisiwa cha Rukuba.
Ndugu Jovin ameongezea kuwa, Wodi hiyo ikikamilika itaondoa usumbufu wa kuwapeleka akina MAMA WAZAZI na WATOTO Hospitali ya Mkoa iliyopo Musoma Mjini. Hiyo ni SAFARI ya BOTI ya takribani masaa wawili (2) kwenye Ziwa Viktoria.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji/Kisiwa cha Rukuba Ndugu Japhary Ibrahim Kibhasa alisema ujenzi huo utaanza Mwezi huu (April 2019) na wanatarajia kuukamilisha ifikapo Mwezi Novemba 2019.
Ndugu Kibhasa ameongeza na kusema kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji/Kisiwa cha Rukuba kwamba wanatambua na kushukuru sana kupokea Michango ya Wadau wa Maendeleo ya Kisiwa cha Rukuba wakiwemo Mbunge wao Prof Sospeter Muhongo, Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dr Vincent Naano Anney na Mkurugenzi Halmashauri ya Musoma Ndugu John Kayombo.
Aidha, Ndugu Kibhasa amewaomba Wadau wengine na wapenda Maendeleo kuungana na Viongozi hao ili kuunga mkono jitihada za Wananchi wa Rukuba katika ujenzi wa Wodi hilo.
OFISI YA MBUNGE WA JIMBO inawakumbusha kwamba:
(i) Sherehe za PASAKA za Jimbo la Musoma Vijijini zitafanyika Kisiwani Rukuba (20-21.04.2019). Wote mnakaribishwa.
(ii) Maktaba ya Shule ya Msingi Rukuba ITAZINDULIWA tarehe 21.04.2019. Mbunge Prof Muhongo ataipatia MAKTABA hiyo VITABU vingi siku hiyo.