WANAVIJIJI WALIKUBALI ZAO JIPYA LA BIASHARA LA ALIZETI JIMBONI MWAO

Moja ya SHAMBA BORA la ALIZETI Kijijini Masinono, Kata ya Bugwema

Na: Hamisa Gamba
Msaidizi wa Mbunge
Wananchi Jimboni Musoma Vijijini wamenufaika na Kilimo cha zao Jipya la ALIZETI lililoanzishwa Jimboni humo na Mbunge wao, Prof Sospeter Muhongo
Akibainisha mafanikio haya mmoja ya WAKULIMA wa ALIZETI Jimboni, Ndugu Tewasa Makunza ambaye ni Mkazi wa Kijiji cha Masinono, Kata ya Bugwema, ameeleza kuwa zao hili la ALIZETI ni zao zuri la BIASHARA lisilo hitaji gharama kubwa kwa Wakulima na kwamba linastahimili UKAME hivyo kuwa na uhakika wa MAVUNO mazuri ukilinganisha na mazao mengine kama Pamba na mengineyo.
Ndugu Makunza ambaye amekuwa akijishughulisha na Kilimo cha zao hili kwa MISIMU MIWILI  iliyopita ameeleza kuwa zao hilo limemuinua zaidi kiuchumi kuliko mazao  mengine ambayo amekuwa akilima, na manufaa zaidi anapokamua MAFUTA, anapata MASHUDU kwa ajili ya MALISHO ya MIFUGO yake.
Ndugu Makunza ameendelea kusema kuwa Idadi ya Mifugo yake hususani, KUKU wameongezeka zaidi katika uzalishaji na ukuaji tangu walipotumia MASHUDU kuwalisha KUKU hao.
Aidha Mkulima huyu (Ndugu Makunza) wa ZAO JIPYA la ALIZETI Musoma Vijijini amekuwa akivuna zaidi ya KILO  1,000 (zaidi ya tani moja) kwa kila msimu. Kwenye Msimu huu amelima EKARI TANO (5) za ALIZETI akitegemea kupata mavuno mazuri.
Zao la ALIZETI ambalo linalimwa Jimboni Musoma Vijijini takribani kwa miaka mitatu (3) sasa, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini amekuwa akitoa MBEGU za ALIZETI BURE kwa Wananchi wa Jimbo lake kama ifuatavyo:
(i) MSIMU WA I: 2016/2017 – Mbunge aligawa kg 4, 682 (Tani 4.68).
(ii) MSIMU WA II: 2017/2018 – Mbunge aligawa kg 4,974 (Tani 4.97).
(iii) MSIMU WA III: 2018/2019 – Mbunge aligawa kg 1, 243.5 (Tani 1.24)
Kwa hiyo kwa ujumla wake Mbunge wa Jimbo Prof Muhongo amegawa bure MBEGU za ALIZETI za jumla ya Kg 9,656 (Tani 9.66) kwa MISIMU 3 mfululizo.
Aidha tunatoa Shukrani kwa Serikali yetu kupitia Wizara ya Kilimo kutupatia TANI KUMI (10) za MBEGU  za ALIZETI kwa ajili ya MSIMU wa Mwaka 2018/2019.
Shukrani za pekee pia zinatolewa kwa Viwanda Vidogo viwili (2) vya Watu Binafsi vilivyokwisha funga MITAMBO yao kwa ajili ya kukamua MBEGU za ALIZETI. Viwanda hivyo ni: SARAGANA OIL MILL kilichojengwa Kijijini Saragana na KUSENYI OIL MILL kilichojengwa Kijijini Kusenyi. Kwa hiyo  SOKO la uhakika liko ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini na kwingineko Mkoani Mara (Bunda na Kiabakari).
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Jitirora cha Kijiji cha Masinono, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, Ndugu Simion Akito, ametoa Shukrani nyingi kwa Mbunge wao Prof Muhongo kwa namna anavyojitolea kwa MAENDELEO ya Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini.
Kata ya Bugwema ndiyo inayoongoza Kata zote 21 kwenye Kilimo cha ALIZETI.
Kilimo ni Uhai
Kilimo ni Biashara
Kilimo ni Ajira