PAROKIA YA BUKIMA YAJENGA MAABARA YA KISASA YA VIPIMO VYA AFYA

Msaidizi wa Mbunge Fedson Masawa akimkabidhi Saruji Paroko Haule katika Parokia ya Bukima

Na: Fedson Masawa
Msaidizi wa Mbunge
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Sospeter Muhongo ametimiza ahadi yake, leo tarehe 06.04.2019, ya kuchangia SARUJI MIFUKO 50 kwa ajili ya Ujenzi wa MAABARA  kubwa ya KISASA ya VIPIMO vya AFYA  inayojengwa katika PAROKIA ya BUKIMA iliyopo Kata ya Bukima.
Awali akifafanua kuhusu ujenzi wa MAABARA hiyo, Kiongozi wa Parokia ya Bukima Padre Haule Emmanuel amesema, MAABARA hiyo itakapokamilika itatoa HUDUMA za KISASA za VIPIMO vya AFYA katika KATA 6 – ambazo ni za Bukima, Bukumi, Bulinga, Bwasi Makojo na Rusoli.
Padre Haule amesema kwa sasa SAMPULI za WAGONJWA za kufanyiwa VIPIMO zinasafirishwa kwenye MABASI kutoka Zahanati za Vijijini hadi kwenye HOSPITAL kubwa ya Musoma Mjini. Huu ni mwendo wa kati ya kilomita 50 na 90 kufika Musoma Mjini.
Padre Haule ameongezea kuwa, kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo, Jengo hilo litakuwa limekamilika kabla ya PASAKA, April 21, 2019 na anamshukuru sana Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Muhongo kwa MCHANGO wake wa SARUJI MIFUKO 50  itakayosaidia kufanikisha ujenzi huo.