WANANCHI WA KATA YA MUGANGO WAWA MFANO WA KUIGWA KWA  KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Ujenzi unaoendelea kwenye Shule ya Sekondari Mugango

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi wa Mbunge
Wananchi wa Kata ya Mugango waendelea kuwa MFANO WA KUIGWA kwenye Miradi ya Maendeleo inayopokea MICHANGO ya SERIKALI kwa ajili ya UTEKELEZAJI wake.
Taarifa ya Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu kwenye Sekondari yao ya Kata (Mugango Secondary School) INATIA MATUMAINI  makubwa.
Sekondari imepokea Tshs Milioni 66.6 kutoka SERIKALINI kwa ajili ya UJENZI wa Vyumba 3 vya Madarasa, Ofisi 1 na Choo chenye Matundu 7 (moja likiwa la Wanafunzi Walemavu).
Wanavijiji, Walimu na Wanafunzi WAMECHANGIA UJENZI huo kama ifuatavyo:
(A) SHULE YENYEWE Walimu na Wanafunzi: (i) wamesomba MORAMU trip 18 (thamani: Tsh 900,000), (ii) wamechangi MITI ya mbao (vipande 88: thamani Tsh 176,000, wameokoa Tsh 1,144,000), (iii) Wamesomba mawe trip 10 (thamani: Tsh 350,000), (iv) Wamesomba maji ya  ujenzi yenye thamani ya Tsh 500,000.
Mwalimu Mkuu Chacha Rugita anatoa makadirio ya Tsh 2,894,000 kuwa thamani ya MCHANGO uliotolewa na WALIMU na WANAFUNZI kwenye ujenzi huu unaoendelea kwenye shule yao.
(B) WANAVIJIJI wakiongozwa na Madiwani wao, Mhe Charles Magoma na Mhe Kadogo Kapi wamechangia: (v) Mchanga trip 40, (vi) Mawe trip 15 na (vii) Kokoto trip 9
MAFANIKIO haya yanatokana na USHIRIKIAKANO MZURI uliopo kati ya WANANCHI (chini ya Uongozi wa Madiwani wao 2 waliotajwa hapo juu), BODI ya Shule (Mwenyekiti Ndugu  Peter Kazimili), na Uongozi wa Shule (Mwalimu Mkuu Ndugu Chacha Rugita).
Mwenyekiti wa BODI ya Shule Ndugu Kazimili ameongezea kuwa, baada ya kukamilisha MRADI huu, wataanza ujenzi wa Miundombinu kwenye Chumba cha Maabara ya BIOLOJIA kwa kutumia SARUJI MIFUKO 50 iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo.
Vilevile Sekondari Mugango wanamshukuru Mbunge wao kwa kuwapatia VITABU vingi na MADAWATI. Wadau wengine wanaoendelea kuchangia Ujenzi na Uboreshaji wa Miundombinu ya Mugango Secondary School ni WANANCHI wakiongozwa na Serikali za Vijiji vyao na Kata yao, kwa kushirikiana kwa karibu sana na Madiwani wao 2, Mhe Charles Magoma na Mhe Kadogo Kapi