SERIKALI YATOA SHILINGI MILIONI 146 KWENYE SHULE YA SEKONDARI KIRIBA

UPAUAJI wa Vyumba vya Madarasa ya Kiriba Secondary School

Na: Verediana Mgoma
Msaidizi  wa Mbunge
Shule ya Sekondari Kiriba iliyoko Kata ya Kiriba imepokea FEDHA kiasi cha SHILINGI MILIONI 146 kwa ajili ya UPAUAJI wa Vyumba Vitatu (3) vya Madarasa. SERIKALI kupitia TAMISEMI imetoa fedha hizo.
Mkuu wa Sekondari hiyo Mwalimu Revocatus Nyesela amesema kuwa Sekondari hiyo ina UPUNGUFU wa Vyumba Vinne (4) vya Madarasa. Kutokana na upungufu huo WANAFUNZI 190 waliochaguliwa kujiunga na KIDATO cha Kwanza (I) kwa sasa wanasomea katika CHUMBA cha MAABARA.
Mwalimu Nyasela AMESHUKURU SANA SERIKALI na kusema kwamba FEDHA HIZO zitaondoa tatizo la upungufu wa Vyumba vya Madarasa shuleni hapo na Chumba cha MAABARA kitatumika kama ilivyokusudiwa.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Kiriba, Ndugu Pendo Isack amesema kuwa kwa sasa WANANCHI wa Kata ya Kiriba WANASHIRIKI VYEMA katika Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa ya Sekondari yao na WAMEKUBALI  ya kuchangia Shilingi Elfu Kumi na Tano (15,000) kwa KILA KAYA.
MICHANGO hiyo ya WANANCHI imesaidia kukamilisha Maboma Matatu (3) ya Madarasa na Ofisi moja (1) ya Walimu ambayo ndiyo yanaezekwa kwa kutumia fedha hizo za Serikali.
Aidha Mtendaji huyo wa Kata hakusita kumpongeza  Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof Muhongo kwa MICHANGO yake ya  kuboresha SEKTA ya ELIMU kwa kuchangia VITABU kwa Shule za Msingi 8 na Sekondari 1,  MADAWATI 362 kwa Shule za Kata hiyo.
Mtendaji aliendelea kutaja MICHANGO ya Mbunge wao ikiwemo SARUJI MIFUKO 120 kwa S/M Kiriba, MIFUKO 120  kwa S/M Chanyauru, MIFUKO 60 kwa S/M Nyamiyenga, na MABATI 54 S/M Bwai.
Fedha za MFUKO wa JIMBO  zilinunua MABATI 106 kwa  S/M Nyamiyenga na S/M Chanyauru.
Aidha  katika kuboresha utoaji wa elimu katika Kata hiyo Afisa Mtendaji huyo amewaomba WADAU wa Maendeleo  kuchangia UJENZI wa HOSTELI unaotarajiwa kuanza hivi karibuni kwa ajili ya WANAFUNZI  wa KIKE ambapo mpaka sasa Wananchi wameanza kujitolea kusomba mawe na mchanga.